Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 5 April 2015

KOMBE LA SHIRIKISHO: KAMUA YANGA! KAMUA USITUMIE HIRIZI!

Kikosi cha Yanga

Na Faustine Feliciane
Licha ya kufungwa 1-0 na Platinum ya Zimbabwe katika mchezo wa marudiano jana, Yanga imekabiza mechi nne kabla ya kukamilisha ndoto ya kocha Hans van der Pluijim ya ya kucheza hatua ya ligi ya Kombe la Shirikisho la klabu za Afrika.

 
Kwa kipigo hicho, Yanga imesonga mbele kwa jumla ya magoli 5-2 hatahivyo hivyo kuingia hatua ya timu 16 bora ya Kombe la Shirikisho.
 
Endapo itavuka raundi ya pili, Yanga itakuwa na kizingiti cha moja ya timu nane zitakazotolewa katika raundi ya tatu ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika kwa ajili ya kuingia robo-fainali ya Kombe la Shirikisho, katikati ya mwaka.
 
Bao la wenyeji Platinum katika mchezo wa jana uliokuwa ukirushwa na televesheni ya Azam lilifungwa katika dakika ya 23 mjini Zvishavane. Timu hiyo ililala 5-1 katika mchezo wa kwanza kwenye Uwanja wa Taifa wiki mbili zilizopita.
 
Baada ya kuonyesha makosa madogomadogo katika dakika 45 za kwanza, Yanga ilirudi uwanjani ikiwa timu tofauti kipindi cha pili na kucheza soka safi kwa muda mwingi wa robo mbili za mwisho wa mchezo. 
 
Na ingeweza kurudi nyumbani na matokeo ya japo sare kama Haruna Niyonzima asingepoteza nafasi nzuri katika kipindi hicho.
 
Akiwa ameingia ndani ya eneo la hatari, na akiwa ameshampiga chenga beki mmoja wa Platinum, Niyonzima alipiga shuti lililokwendan je ya lango la wenyeji.
 
Kusonga mbele kwa Yanga ni hatua moja zaidi kuliko mwaka jana ilipotolewa na Al Ahly ya Misri katika raundi ya kwanza ya michuano mikubwa zaidi ya ngazi ya klabu Afrika.
 
Timu hizo zilishinda 1-0 kila moja nyumbani kabla ya Yanga kuaga kwa mikwaju ya penalti jijini Cairo.
 
Baada ya mafanikio hayo katika anga ya kimataifa, akili ya Yanga inarudi kwenye ligi kuu ya Bara haraka ambako timu hiyo itakuwa mwenyeji wa Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa Jumatano.
 
Yanga (40) inaongoza ligi kuu ya Bara kwa tofauti ya pointi nne juu ya Azam yenye mechi moja mkononi na ambayo itaikaribisha Mbeya City kwenye Uwanja wa Azam Complex Jumatano pia.
 
Katika mechi za ligi kuu ya Bara jana, mchezo kati ya Kagera Sugar na Simba uliahirishwa kutokana na maji ya mvua kujaa kwenye Uwanja wa Kambarage, wakati Ndanda na City zilitoka sare ya 1-1, Ruvu Shooting ikaifunga JKT Ruvu 1-0 kwenye Uwanja wa Mabatini.
 
Goli hilo lilifungwa na Yahaya Tumbo katika dakika ya 54 kutokana na krosi ya Michael Aidan. Ni goli la tano kwa mchezaji huyo tangu asajiliwe Desemba mwaka jana.
 
Kwenye Uwanja wa Mkwakwani, wenyeji Coastal walilizwa 1-0 na Prisons mfungaji akiwa Jeremia Juma katika dakika ya 45.   
 
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment