Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 19 June 2015

TWFA KUFANYA UCHAGUZI AGOSTI 15

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA), George Mushumba ametangaza uchaguzi mkuu wa chama hicho utakaofanyika agosti 15, 2015 kujaza nafasi mbalimbali.

Kwa mamlaka aliyonayo anapenda kutangaza uchaguzi mkuu wa TWFA leo kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi, uchaguzi huo utafanyika tarehe 15, Agosti 2015 katika nafasi zifuatazo:

  1. Mwenyekiti
  2. Katibu Msaidizi
  3. Mweka Hazina
  4. Wajumbe wawili wa Kamati ya Utendaji.       

Fomu za kuomba nafasi hizo zitaanza kutolewa tarehe 19-23 Juni 2015 katika ofisi za TFF zilizopo Karume jijini Dar es salaam.

Kalenda ya Uchaguzi wa TWFA imeambatanishwa:

JEDWALI NAMBA MOJA (1)
KALENDA YA MATUKIO YA UCHAGUZI YA TWFA


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

No comments:

Post a Comment