Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 29 September 2015

WANAMUZIKI WAKAMATWA SOMALILAND

Wanamuziki wa Somaliland wanaruhusiwa kutumbuiza popote ulimwenguni isipokuwa Somalia
Wanamuziki maarufu wa Somaliland, the Horn Stars, wamekamatwa wakituhumiwa kupunga bendera ya Somalia kwenye Tamasha.

Kundi hilo lilikuwa likitumbuiza katika sikukuu ya Eid al-Adha mjini Mogadishu nchini Somalia.
Wanamuziki wanne wanatuhumiwa kutumbuiza kwa nyimbo zinazopinga uhuru wa Somaliland.
Somaliland ilijitangazia uhuru wake kutoka Somalia mwaka 1991 lakini haijatambuliwa kimataifa.
Wanamuziki hao walikamatwa wakati waliporejea Somaliland katika mji mkuu wa nchi hiyo, Hargeisa siku ya jumapili.
Katika mtandao wa Twitter watu wameanza kutoa maoni yao wakitaka wanamuziki hao kuachiwa huru.
Naibu waziri wa mambo ya ndani wa Somali land Ahmed Adarre amesema ''Wasanii wanaweza kutumbuiza popote duniani lakini sio Somalia.hivyo hawapaswi kujihusiaha na siasa'' alieleza.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment