Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday, 13 August 2015

PAULO WANCHOPE ABWAGA MANYANGA COSTA RICA KWA KUPIGANA

Paulo Wanchope

Meneja wa timu ya taifa ya mpira wa miguu wa Costa Rica, Paulo Wanchope, amebwaga manyanga siku moja baada ya kuhusika na tukio la kupigana wakati wa mchezo huko Panama.
Paulo Wanchope mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Costa Rica aliyewahi pia kucheza kwenye ligi kuu nchini Uingereza, alikuwa akitazama timu yake ya taifa ya vijana walio chini ya miaka (23) wakati vurumai hizo zilipozuka.
Paulo anaonekana katika mkanda wa video akiwa na hasira huku akifungua geti karibu na uwanja ambapo alianza kupambana na bwana mmoja kabla ya wanausalama kuingilia kati.
Vyombo vya habari nchini humo vimesema kuwa meneja huyo hakua na furaha na muamuzi wa mchezo huo,pamoja na hayo mchezo huo uliisha kwa matokeo ya bila kufungana.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment