Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 23 August 2015

WEST BROM YANYUKWA 3-2 NA CHELSEA


Chelsea wanasajili ushindi muhimu wa mabao 3-2 dhidi ya West Brom ugenini.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na kiungo mgeni kutoka Uhispania Pedro katika dakika ya 20 ya kipindi cha kwanza.


Costa aliifungia chelsea bao la pili

Hii ndiyo iliyokuwa mechi yake ya kwanza tangu ajiunge na 'the Blues'' katikati ya juma hili.
West Brom watajilaumu wenyewe baada yao kupoteza fursa ya kuilaza Chelsea mapema walipopoteza penalti.

James Morrison alipiga mkwaju hafifu na kipa Courtois hakufanya masihara nao

James Morrison alipiga mkwaju hafifu na kipa Courtois hakufanya masihara nao.
Courtois ambaye alikuwa anacheza mechi yake ya kwanza tangu aoneshwe kadi nyekundu majuma mawili yaliyiopita alikuwa na kila sababu ya kutabasamu na kumfanya kocha Mourinho amsamehe kwa makosa yaliyopelekea yeye kutimuliwa.
Hata hivyo Diego Costa aliongezea matumaini ya the Blues kusahau kichapo walichopata majuzi alipofanya mambo kuwa mabao mawili kwa nunge kunako dakika ya 30.

César Azpilicueta

West Brom waliendelea kuuliza safu ya ulinzi ya Chelsea maswali na wakapata majibu kunako dakika ya 35 Morrison aliporekebisha makosa yake na kuifungia West Brom bao lao la kwanza.
César Azpilicueta alimhakikishia Mourinho alama zote tatu muhimu kwa bao lake la dakika ya 42.
James Morrison aliendelea kuwa mwiba katika safu ya ulinzi ya Chelsea .
Gonga gonga yake ilisababisha bao la pili kwa mkwaju wa kichwa.

Terry aoneshwa kadi nyekundu

West Brom waliendelea kufanya mashambulizi na shinikizo lao likasababisha Kiungo wa Chelsea John Terry kuoneshwa kadi nyekundu kwa kumburura Salomón Rondón.
Mwisho wa kuishia The Blues wanarejea darajani wakiwa wametia kibindoni alama tatu muhimu.
Chelsea wanasajili ushindi muhimu dhidi ya West Brom ugenini.
Mpira umekwisha.
90:02
West Brom 2-3 Chelsea ''
John Obi Mikel anaingia uwanjani kuchukua pahala pa Pedro
83:02
Freekick kwa upande wa Chelsea (Pedro)
82:13 West Brom 2-3 Chelsea
West Bromwich Albion wanajipatia kona Branislav Ivanovic.

Gary Cahill

70:13
Gary Cahill akiwa amevalia barakoa baada ya kujeruhiwa pua
Je uamuzi wa refarii Mark Clattenburg kutoa kadi nyekundu umekurithisha ?

Je uamuzi wa refarii Mark Clattenburg kutoa kadi nyekundu umekurithisha ?

65:28 West Bromwich Albion 1- 3 Chelsea
GOOOOOOOL
James Morrison anafungia West Brom bao la pili kwa kichwa
58:34West Brom 2-3 Chelsea
West Bromwich Albion 1- 3 Chelsea

Terry

53:21 John Terry (Chelsea) anaoneshwa kadi nyekundu
50:34
West Bromwich Albion 1- 3 Chelsea
46:41
Kona kuelekea lango la Chelsea
45:00 Pedro anaunawa mpira

West Bromwich Albion 1, Chelsea 3.

West Bromwich Albion 1, Chelsea 3.
Kipindi cha pili kimeanza
Kipindi cha kwanza kimekamilika hapa The Hawthorns
Matokeo ni West Bromwich Albion 1- 3 Chelsea

West Bromwich Albion 1- 3 Chelsea

45:00
West Bromwich Albion 1- 3 Chelsea
41:40 Goal scored
Goooooooooool!

Bao la tatu la Cesar Azpilicueta

West Bromwich Albion 1- 3 Chelsea
César Azpilicueta
30:00
West Bromwich Albion 0, Chelsea 2

West Bromwich Albion 0, Chelsea 2

29:01
GOOOOOOL Diego Costa anaifungia chelsea bao la pili West Bromwich Albion 0, Chelsea 2 ''
24:01

Courtois akiokoa penalti

West Brom 0-1 Chelsea
19:30
GOOOOOOOOAL


Pedroooooo
Pedro akifungua akaunti yake Chelsea
West Brom 0-1 Chelsea

Courtois

17:45 West Brom 0-0 Chelsea
Freekick kuelekea lango la Chelsea
Callum McManaman (West Bromwich Albion) anachezewa visivyo
16:11
Nemanja Matic (Chelsea) anaoneshwa kadi ya njano
12:35 LOOOOOOO
Penalti inaokolewa hapa

Courtois ameokoa penalti

Amini usiamini James Morrison wa West Bromwich Albion anapiga mpira hafifu na kipa nambari moja Courtois anathibitisha kwanini yeye ndiye anayepewa majukumu langoni
12:27 Penalti kuelekea lango la Chelsea
Nemanja Matic anacheza visivyo
5:03 West Brom 0-0 Chelsea

Mechi imeanza

Diego Costa anafanya mashambulizi ya mapema mbele ya lango la wenyeji wao
3:21
West Brom v Chelsea

Kocha Tony wa West Brom

Salomón Rondón wa West Bromwich Albion anamjaribu kipa wa Chelsea Courtios
Mechi imeanza kwa kishindo

Timu ya West Brom

West Bromwich Albion
13 Myhill 25 Dawson 23 McAuley 03 Olsson 11 Brunt 24 Fletcher 05 Yacob 19 McManaman 14 McClean 07 Morrison 33 Rondón

Mashabiki wameanza kuwasili hapa uwanjani

Wachezaji wa akiba
04 Chester 06 Lescott 08 Gardner 10 Anichebe 17 Lambert 31 Gnabry 38 Rose

Timu ya Chelsea

Kikosi cha Chelsea;
13 Courtois 02 Ivanovic 26 Terry 05 Zouma 28 Azpilicueta 04 Fàbregas 21 Matic 17 Pedro 22 Willian 10 Hazard 19 Diego Costa
Wachezaji wa akiba

Pedro aliyesajiliwa majuzi na Chelsea

01 Begovic 09 Falcao 12 Mikel 14 Traore 18 Remy 24 Cahill 36 Loftus-Cheek
Victor Moses na Oscar, hawatakuwa uwanjani baada ya kuripotiwa kujeruhiwa mazoezini

Bila shaka Kocha Jose Mourinho angependa kusahau matokeo ya mechi yao ya mwisho

Kocha Jose Mourinho anajivunia kiungo mpya Pedro

Kocha Mourinho

Chelsea wanahitaji ushindi kwa udi na uvumba ilikufufua kampeini yao msimu huu.

Kikosi cha utabibu cha Chelsea

Bila shaka Mourinho angependa kugonga vichwa vya Habari kwa kushinda wala sio kutofautiana na kitengo cha utabibu

Kipa Courtois aliyeonesha kadi nyekundu anarejea uwanjani leo

Karibu katika matangazo ya moja kwa moja kati ya West Brom na Chelsea.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment