Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 19 August 2015

WAHAMIAJI 107,000 WALIINGIA ULAYA JULAI PEKEE

Baadhi ya wahamiaji walionusurika kifo wakati wakiingia Ulaya 
Shirika la Umoja wa Ulaya linalopambana na maswala ya uhamiaji haramu na biashara ya binadamu, Frontex limetoa wito kwa nchi wanachama wa umoja huo kutoa msaada zaidi kwa nchi tatu zilizoathirika kutokana na kuwa na idadi kubwa ya wahamiaji.

Ugiriki, Italia na Hungary ni nchi zinazoelezwa kuathiriwa zaidi.
Shirika hilo limetaja hali hiyo kuwa ya dharula na kutoa wito wa kuongezwa kwa maofisa na vifaa zaidi ili kushughulikia tatizo hilo.
Frontex imesema mwezi uliopita zaidi ya Watu 107,000 waliwasili ulaya kwa njia za panya, ikiwa ni mara tatu zaidi ya waliowasili mwezi Julai mwaka jana.
Watu hao wengi wanaelezwa kutoka nchini Syria,Afghanistan na nchi za kusini mwa jangwa la Sahara wakikimbia hali mbaya ya usalama na umasikini
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment