Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday, 16 August 2015

WAFUASI WA DADIS CAMARA WASHAMBULIWA GUINEA

Moussa Dadis Camara
Polisi nchini Guinea wamepambana na wafuasi wa aliyekuwa kiongozi wa kijeshi wa nchi hiyo Moussa Dadis Camara.
Takriban watu 2000 walikuwa wamekusanyika katika uwanja wa ndege kwenye mji mkuu wa Conakry kufuatia uvumi kwamba bwana Camara angerejea nyumbani kutoka uhamishoni.
Wengi waliondoka baada ya saa kadhaa lakini kundi dogo lilikataa kuondoka.
Bwana Camara amesema kuwa ana nia ya kuwania urais ambao unapangiwa kufanyika mwezi Oktoba licha ya kuhukumiwa mwezi uliopita kwa kuhusika kwenye mauaji ya zaidi ya waandamanaji 156 miaka sita iliyopita.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment