Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday, 18 August 2015

MAKUNDI YAMEKWISHA, MEMBE NA WAGOMBEA 8 WALIOSHINDWA URAIS CCM KUMNADI DK. MAGUFULI


Dk. John Pombe Magufuli (kulia), akigonga na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, wakati wa mkutano mkuu wa CCM mjini Dodoma Julai 12, 2015 uliompitisha kuwa mgombea urais.

Na Daniel Mbega wa www.brotherdanny.com
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimeyavunja makundi na kuweka mshikamano kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 hasa baada ya kuona upinzani umepata nguvu kubwa tangu Edward Lowassa alipokimbilia Ukawa baada ya kutemwa Dodoma.
Na katika kudhihirisha kwamba CCM wameungana, Halmashauri Kuu ya chama hicho iliyokutana jijini Dar es Salaam katika kikao cha siku moja Agosti 17, 2015 imeunda Kamati ya Kampeni itakayomnadi mgombea wake Dk. John Pombe Joseph Magufuli.
Ndani ya kamati hiyo yenye wajumbe 32, wamo makada tisa ambao waligombea urais pamoja na Dk. Magufuli na wakashindwa pamoja na Lowassa.
NEC, iliyokuwa chini ya mwenyekiti wake Dk. Jakaya Kikwete, iwateua Bernad Membe, January Makamba na Dk. Asha-Rose Mtengeti Migiro ambao walipenya kwenye tano bora pamoja na Dk. Magufuli huku Dk. Migiro akifika fainali.
Wengine waliowania urais ambao sasa wamekabidhiwa jukumu la kumnadi Dk. Magufuli ni Waziri wa Uchukuzi Samwel Sitta, Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba, Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu, Waziri wa Afrika Mashariki Dk. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Steven Wasira na Mbunge wa Afrika Mashariki Charles Makongoro Nyerere.
Wajumbe wengine kwenye kamati hiyo muhimu ni Abdulrahman Kinana (Mwenyekiti), Rajab Luhwavi (Makamu Mwenyekiti – Bara), Vuai Ali Vuai (Makamu Mwenyekiti - Z’bar), Sofia Simba, Mohamed Seif Khatib, Nape Nnauye, Amina Makillagi, Christopher Ole Sendeka, Abdallah Majura Bulembo, Hadija Aboud, Mohamed Aboud, Issa Haji Ussi, Waride Bakari Jabu na Mahmoud Thabit Kombo.
Wengine ni Shamsi Vuai Nahodha, Maua Daftari, Stephen Masele, Pindi Chana, Shaka Shaka, Sadifa Juma Khamis, Antony Diallo, Livingston Lusinde na Ummy Mwalimu.
Kwa namna mchakato wa kuwania uteuzi wa kugombea urais ulivyokuwa na figisu figisu, kuteuliwa kwa wajumbe hao tisa, ambao nao walikuwa na kambi zilizokuwa zinasigana, kunamaanisha kwamba makundi hayo yamezikwa rasmi na sasa wote wamekuwa chama kimoja kuhakikisha kwamba wanasaidia ili kiendelee kutawala.
Kuondoka kwa Lowassa pamoja na makada wengi na wanachama kuelekea Chadema, kwa kiasi kikubwa kumeifumbua macho CCM na kuona kwamba kama itaendelea na msuguano inaweza kujikuta katika wakati mgumu, hasa kutokana na vuguvugu kubwa la mageuzi lililopo upande wa pili.
Ingawa haijajulikana majukumu ya kamati hiyo, lakini ni wazi kwamba ndiyo itakayohusika na uratibu na utekelezaji wa shughuli zote za kampeni za urais pamoja na kuweka mikakati thabiti ya kushinda viti vingi vya udiwani na ubunge, ambavyo vinatishiwa na ujio wa Lowassa ndani ya Ukawa.
Wagombea urais wengine ambao ni wazi pia watakuwa wameungana licha ya kutoteuliwa kwenye kamati hiyo walikuwa Dk. Titus Kamani ambaye ameshindwa kwenye kura za maoni Busega, Profesa Sospeter Muhongo, Balozi Amina Salum, Profesa Mark Mwandosya, Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye, Waziri Mkuu wa sasa Mizengo Pinda, William Ngeleja, Peter Nyalali, Dk. Khamis Kigwangalla, Luhaga Mpina ambaye amekosa mpinzani ndani ya CCM katika Jimbo la Kisesa.
Wengine walikuwa Dk. Augustine Mahiga, Dk. Mwele Malecela, Elidephonce Bihole, Dk. Hassy Kitine, Joseph Chagama, Balozi Ali Karume, Maliki Malupu, Dk. Mohamed Ghalib Bilal, Amos Siyantemi, Jaji Augustino Ramadhani, Dk. Mussa Kalokola, Ritta Ngowi, Monica Mbega, Nicholas Mulenda, Banda Sonoko, Helen Elinawinga, Mathias Chikawe, Antony Chalamila, Veronica Kazimoto na Peter Nyalali.


(Imeandaliwa na www.brotherdanny.com)

No comments:

Post a Comment