Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 24 May 2015

KABURI LA PAMOJA LA WAHAMIAJI LAPATIKANA

Kaburi la pamoja lapatikana jirani na kambi za wahamiaji.
Utawala nchini Malaysia unasema kuwa umegundua kaburi la pamoja karibu na kambi za kusafirisha watu kimagendo zilizoachwa karibu na mpaka kati ya nchi hiyo na Thailand.

Ripoti za vyombo vya habari zinasema kuwa makaburi hayo yaliogunduliwa wiki iliyopita huenda yakawa na takriban miili 100 inayokisiwa kuwa ya wahamiaji kutoka nchini Myanmar na Bangladesh.
Waziri wa masuala ya ndani wa Malaysia aliviambia vyombo vya habari kuwa ameshangazwa kugundua kuwa huenda kambi hizo zimekuwa eneo hilo kwa miaka mitano.
Mapema mwezi huu makaburi kama hayo yanayoaminika kuwa ya wahamiaji yaligunduliwa eneo lililo kusini mwa Thailand.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment