Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday, 16 June 2014

SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA WATOTO WA MITAANI YAGUBIKWA NA MACHOZI YA KUBAKWA

Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Arusha

IKIWA leo ni Siku ya Mtoto wa Afrika baadhi ya watoto wa mitaani ambao hawana makazi maalumu katika jiji la Arusha wamewalaumu baadhi ya wazazi wasio waaminifu ambao wakati mwingine huwageuza kinyume cha maumbile na kisha kuwapa ujira  wa kiasi cha shilingi mia tano.
Watoto hao walitoa kilio hicho mapema leo pembezoni mwa uwanja wa mpira wa sheikh amri abeid ambapo ndipo maskani yao wakati wakiongea na Brother Danny Blog kuhusiana na uhuru wao.

Walidai kuwa watu wazima wakati wa usiku huwa wana warubuni tena watoto wa kiume kwa kuwadanganyana kisha kuwaaangilia kinyume cha maumbile na kisha kuwapa kiasi cha shilingi mia tano mpaka elfu moja.

Walisema kuwa kutokana na ugumu wa maisha wakati mwingine wanalazimika kufanya hivyo kwa kuwa hawana mahitaji muhimu ingawaje wanapata wakati mgumu wa maumivu.
"Hawa watu wazima ni wale ambao ni matajiri kabisa tena vigogo wa Jiji la Arusha na tunawajua kabisa ila wanatuambia kuwa tukifanya hivyo watatusaidia sana ila ndio nyimbo zao za kila siku au kama wakati mwingine wasipotoa kiasi hicho wanatupa vyakula au nguo nguo sasa sisi tunaumia," waliongeza hivyo.
Pia walidai kuwa mbali na kujikuta wakiwa wanageuzwa kinyume cha maumbile na kisha kupata maumivu makali wakati mwingine pia wanalazimika kujisaidia haja kubwa ndani ya mifuko na kisha kuitupa kwenye mitaro japokuwa jiji linapambana na usafi .
Kutokana na hilo waliomba uongozi wa Jiji kuhakikisha kuwa wanawaaangalizia msaada hata wa choo ili waweze kujisaidia kwani kwa kufanya hivyo wataweza kuboresha mazingira na kisha kuyaweka katika mazingira ya usafi zaidi tofauti na sasa.
"Ukiingia katika vyoo vya kujisaidia unalazimika kulipa kiasi cha shilingi 200 sisi hatuna hiyo pesa kwahiyo tunachukua malboro na kisha kujisaidia humo humo je sasa hapo tunajenga au tunabomoa mazingira  msaada ni muihimu na pia wazazi nao majumbani wanatakiwa kupewa elimu ya kuishi na watoto hasa mayatima kwani wao ndio chanzo kikubwa cha sisi kuongezeka hapa Arusha," waliongeza watoto hao.

No comments:

Post a Comment