
Shabiki makini: Mchumba wa Mario Balotelli, Fanny Neguesha alikuwa miongoni mwa mashabiki wa Italia dhidi ya England.
MSHAMBULIAJI mtukutu, Super Mario Balotelli macho yake hayakuwa kwa taifa lake tu, bali hata kwa mchumba wake Fanny Neguesha ambaye alikuwa miongoni mwa mashabiki waliofurika katika mchezo wa ufunguzi wa Italia wa kundi D dhidi ya Simba watatu, timu ya taifa ya Engaland.
Katika mechi hiyo ambayo Balotelli aliifungia Italia bao katika ushindi wa 2-1, mchuchu wa nyota huyo alivalia jezi namba 9 ya Italia yenye jina la basha wake, Balotelli.
Neguesha kwa muda wote alikuwa na tabasamu baada ya mpenzi wake kufunga bao safi kwa kichwa mapema kipindi cha pili na kuifanya Italia iwe mbele kwa mabao 2-1.
Kutazama picha zaidi za mchumba wa Balotelli bofya www.bkmtata.blogspot.com
CHANZO FULL SHANGWE
No comments:
Post a Comment