Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday, 15 June 2014

KUMEKUCHA KOMBE LA DUNIA, TEMBO WA AFRIKA WAICHABANGA JAPAN 2-I, BONY, GERVINHO VIDUME!

Kneesy does it: Ivory Coast's forward Gervinho celebrates with Didier Drogba after putting his side 2-1 upNyota wa  Ivory Coast  Gervinho akishangilia bao lake na  Didier Drogba. 
 
MAGOLI mawili ya vichwa  ya Wilfried Bony na Gervinho yaliyopishana kwa sekundi 98 yameipa ushindi wa kwanza Ivory Coast kwenye mchezo wa kundi la C wa kombe la dunia na kuilaza Japan mabao 2-1 mjini Recife.
Bony aliifungia Ivory Coast bao la kusawazisha katika dakika ya 64 na Gervinho akaongeza bao la ushindi mnamo dakika ya 66.
Japan walikuwa wa kwanza kuandika bao katika dakika ya 16 ya kipindi cha kwanza kupitia kwa nyota wao Keisuke Honda, na baada ya hapo Ivory Coast waliendelea kupoteza nafasi za kufunga.
Kutokana na uzembe huo wa washambuliaji wa Ivory Coast ilionekana ndoto ya kufuzu hatua ya 16 kutoka kundi C inaweza kupotea kutokana na ushindi waliopata Colombia dhidi ya Ugiriki katika kundi lao la C.
 Tembo hao kutoka pwani ya magharibi mwa Afrika walimuacha nahodha wao , Didier Drogba katika kikosi kilichoanza ambapo aliingia katika dakika ya 62 akichukua nafasi ya Die na alifanya vizuri kwa dakika hizo alizocheza.
Turning it around: Gervinho and Wilfried Bony scored two goals in two minutes to put Ivory Coast aheadGervinho na Wilfried Bony walifunga mabao mawili ndani ya dakika mbili na kuwapa ushindi Ivory Coast.

Kusoma zaidi na kutazama picha za mechi hii bofya www.bkmtata.blogspot.com.

CHANZO FULL SHANGWE

No comments:

Post a Comment