Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa skafu mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Usindi wilayani Kaliua mahali ambapo amepokelewa.Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wana CCM pamoja na wananchi mara baada ya kuwasili KaliuaMh. Samwel Sitta Mbunge wa jimbo la Urambo Mashariki na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisalimiana na Profesa Juma Kapunya Mbunge wa jimbo la Urambo Magharibi leo asubhui katika kijiji cha Usindi kata ya Ushokora wilayani Kaliua wakati wa pamokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitokea Wilaya ya Urambo.Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa Prisca Kaholwe Ofisa mtendaji wa kijiji cha Uhuru wilayani Urambo wakati alipokagua ujenzi wa Zahanati ya kijiji hicho.Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na viongozi mbalimbali wa a CCM wilayani Kaliua wakielekea kwenye ukaguazi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa Zahanati ya Kijiji cha Usindi Kata ya Ushokora wilayani Kaliua.Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika ujenzi wa nyumba za watumishi wa zahanati ya kijiji cha Usindi.Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiendelea na ukaguzi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa katika zahanati ya Usindi nyuma yake ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi.Jengo la zahanati ya Usindi kata ya Ushokora ambalo limekamilika lakini bado halijaanza kazi kwa visingizio vya kutokuwepo nyumba za watumishi.
CHANZO FULL SHANGWE
No comments:
Post a Comment