KESI namba 306/13 inayomkabili Nabii na Mtume wa Kanisa la Ephata la
Dar, Josephat Mwingira, ya kuzaa na mke wa mtu, Alhamisi iliyopita
iliunguruma mahakamani na kusababisha watu kufurika wanaoaminika kuwa ni
waumini wake.
Mlalamikaji katika kesi hiyo, Dokta William Morris alimfungulia kesi Nabii Mwingira katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam akimtuhumu kuzaa na mkewe.
Kesi hiyo ilipoanza kuunguruma, Nabii Mwingira aliwakilishwa na Wakili Moses Kaluwa ili ikiwezekana amnasue kwenye aibu hiyo.
Shauri hilo lipo mbele ya Hakimu Hellen Riwa na upande wa mlalamikaji ukiwakilishwa na Wakili Musa Mwapongo.
Hakimu Riwa baada ya kuitaja kesi hiyo aliutaka upande wa utetezi kuwasilisha utetezi wao mahakamani hapo Desemba 30 mwaka huu ambapo Januari 22 mwakani itatajwa tena.
Kesi hiyo ya aina yake, iliyohudhuriwa na umati unaoaminika ni wafuasi wake Mwingira, ilisababisha hakimu aliyekuwa akiisikiliza, kuwaamuru mawakili na wangine waliovaa makoti kuyavua kutokana na joto kali lililosababishwa na watu kufurika ndani ya mahakama.
Baada ya kesi hiyo kuahirishwa baadhi ya waumini wake Mwingira walionekana kupigwa butwaa ambapo mmoja alionekana kutoamini alichokisikia mahakamani. “Nilikuja kuthibitisha kama kweli Uwazi (gazeti hili) lilisema kweli kuwa kuna kesi hii… inasikitisha sana,” alisikika akisema.
CHANZO: http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/kesi-ya-mwingira-mahakama-yajaa-waumini-wake
Mlalamikaji katika kesi hiyo, Dokta William Morris alimfungulia kesi Nabii Mwingira katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam akimtuhumu kuzaa na mkewe.
Kesi hiyo ilipoanza kuunguruma, Nabii Mwingira aliwakilishwa na Wakili Moses Kaluwa ili ikiwezekana amnasue kwenye aibu hiyo.
Dk. Philis Nyimbi anayedaiwa kuzaa na Nabii Mwingira.
Shauri hilo lipo mbele ya Hakimu Hellen Riwa na upande wa mlalamikaji ukiwakilishwa na Wakili Musa Mwapongo.
Hakimu Riwa baada ya kuitaja kesi hiyo aliutaka upande wa utetezi kuwasilisha utetezi wao mahakamani hapo Desemba 30 mwaka huu ambapo Januari 22 mwakani itatajwa tena.
Kesi hiyo ya aina yake, iliyohudhuriwa na umati unaoaminika ni wafuasi wake Mwingira, ilisababisha hakimu aliyekuwa akiisikiliza, kuwaamuru mawakili na wangine waliovaa makoti kuyavua kutokana na joto kali lililosababishwa na watu kufurika ndani ya mahakama.
Baada ya kesi hiyo kuahirishwa baadhi ya waumini wake Mwingira walionekana kupigwa butwaa ambapo mmoja alionekana kutoamini alichokisikia mahakamani. “Nilikuja kuthibitisha kama kweli Uwazi (gazeti hili) lilisema kweli kuwa kuna kesi hii… inasikitisha sana,” alisikika akisema.
CHANZO: http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/kesi-ya-mwingira-mahakama-yajaa-waumini-wake
No comments:
Post a Comment