Pages

Pages

Pages

Sunday 12 January 2014

NABII MWINGIRA KUZAA NA MKE WA MTU...


KESI namba 306/13 inayomkabili Nabii na Mtume wa Kanisa la Ephata la Dar, Josephat Mwingira, ya kuzaa na mke wa mtu, Alhamisi iliyopita iliunguruma mahakamani na kusababisha watu kufurika wanaoaminika kuwa ni waumini wake.

Mtume na Nabii Josephat Mwingira.

Mlalamikaji katika kesi hiyo, Dokta William Morris alimfungulia kesi Nabii Mwingira katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam akimtuhumu kuzaa na mkewe.
Kesi hiyo ilipoanza kuunguruma, Nabii Mwingira aliwakilishwa na Wakili Moses Kaluwa ili ikiwezekana amnasue kwenye aibu hiyo.
Dk. Philis Nyimbi anayedaiwa kuzaa na Nabii Mwingira.

Shauri hilo lipo mbele ya Hakimu Hellen Riwa na  upande wa mlalamikaji ukiwakilishwa na Wakili Musa Mwapongo.
Hakimu Riwa baada ya kuitaja kesi hiyo aliutaka upande wa utetezi kuwasilisha utetezi wao mahakamani hapo Desemba 30 mwaka huu ambapo Januari 22 mwakani itatajwa tena.

Kesi hiyo ya aina yake, iliyohudhuriwa na umati unaoaminika ni wafuasi wake Mwingira, ilisababisha  hakimu aliyekuwa akiisikiliza, kuwaamuru mawakili na wangine waliovaa makoti kuyavua kutokana na joto kali lililosababishwa na watu kufurika ndani ya mahakama.
Baadhi ya waumini wa Mwingira wakiwa eneo la mahakama.

Baada ya kesi hiyo kuahirishwa baadhi ya waumini wake Mwingira  walionekana kupigwa butwaa ambapo mmoja alionekana kutoamini alichokisikia mahakamani. “Nilikuja kuthibitisha kama kweli Uwazi (gazeti hili) lilisema kweli kuwa kuna kesi hii… inasikitisha sana,” alisikika akisema.

CHANZO: http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/kesi-ya-mwingira-mahakama-yajaa-waumini-wake

No comments:

Post a Comment