Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 11 January 2017

MWIMBAJI MPYA WA INJILI KANDA YA ZIWA, JIMMY GOSPO, AACHIA WIMBO WAKE RASMI

Na George Binagi @BMG
Jimmy Gospo (pichani) ni mwanamziki mpya kwenye muziki wa injili nchini Tanzania. Kabla ya mwaka 2014 alikuwa akifanya muziki wa Bongo Fleva, akiwakilisha mkoa wa Geita na Kanda ya Ziwa kwa ujumla.


Baada ya mwaka 2014, Jimmy Gospo aliamua kugeuza uelekeo na kuanza kuimba nyimbo za injili kwenye matamasha mbalimbali ya injili hususani Kanda ya Ziwa. Baada ya hapo alianza kurekodi albamu yake ambayo hadi sasa jina liko kampuni.


Mwaka huu 2017 ameanza kuachia rasmi baadhi ya nyimbo zilizo kwenye albamu hiyo. Ameanza na wimbo uitwao "Nakujua Bwana" ambao hakika ni wimbo bora kusikiliza na hata mafundisho yake.


"Ni nyimbo nzuri kwa watu wengi hasa wale ambao tunatamani kuisikia faraja ya Bwana ikitenda na sisi. Niwakaribisheni watanzania wote tuisikilize Ninakujua Bwana, ni nyimbo nzuri na natumaini utaifurahia na kuipenda". Amesisitiza Jimmy.

Mwimbaji wa muziki wa injili, Jimmy Gospo (kulia), akizungumza na George Binagi-GB Pazzo wa BMG (kushoto), kuhusiana na ujio wake kwenye muziki huo, baada ya kuachana na muziki wa kidunia.
Sikiliza Mahojiano Hapa kusikiliza mahojiano.

No comments:

Post a Comment