Pages

Pages

Pages

Wednesday 3 August 2016

ABIRIA 282 NA WAHUDUMU 18 WA NDEGEYA EMIRATES WANUSURIKA KIFO, NI BAADA YA NDEGE KUWAKA MOTO BAADA YA KUTUA HUKO DUBAI


NA K-VIS MEDIA NA MASHIRIKA YA HABARI
Shughuli ZOTE KWENYE UWANJA WA NDEGE WA Kimataifa wa Dubai, Himarati, zimesimama baada ya ndege iliyobeba abiria 300, kupata hitilafu ilipotua na kasha kuwaka moto.
Ndege hiyo Emirates Boeng 777 ilikuwa ikisafiri kutoka Thiruvananthapuram nchini India wakati ilipokumbwa na mkasa huo mapema leo Agosti 3, 2016.
Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari, abiria wote 282 na wahudumu wa ndege 18 wa ndege hiyo chapa EK521 waliokolewa na wako salama ukiachilia mbali mishtuko kutokanana dhahma hiyo.
Mamlaka za Dubai hazijatoa maelezo zaidi kuhusiana na ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment