Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 1 August 2015

WAHAMIAJI 2,000 WANASWA WAKIJIANDIKISHA KUPIGA KURA


Idara ya uhamiaji nchini imesema inawashikilia wahamiaji haramu 2,048 kutoka nchi mbalimbali kwa tuhuma za kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura.
Naibu kamishna wa uhamiaji na msemaji mkuu wa idara hiyo, Abbas Mussa alisema jana kuwa wahamiaji hao wanatoka nchi za Kenya, Burundi na Uganda.
Alisema walikamatwa katika mikoa 14 wakijifanya ni Watanzania, lakini ilibainika kuwa siyo raia baada ya idara hiyo kufanya uchunguzi kwenye vituo vya uandikishaji.
“Baadhi yao tumewafikisha mahakamani, lakini wengine bado uchunguzi unaendelea na wakibainika nao watachukuliwa hatua,” alisema Mussa.
Aliongeza kuwa wengi ya wahamiaji hao walifika mikoa ya Kagera, Mara, Tanga, Kigoma, Rukwa, Kilimanjaro, Ruvuma, Geita, Shinyanga, Mtwara, Pwani, Mbeya, Morogoro na Dar es Salaam.
“Inasikitisha sana, kwani baadhi ya waliokamatwa walishajiandikisha na kupewa vitambulisho kama raia wa Tanzania,” alisema.
Alisema kutokana na hali hiyo, Idara imeamua kuongeza maofisa katika vituo ili kuendelea kuwabaini wahamiaji hao.
Mussa aliwataka wananchi kutoa taarifa mara wanapobaini watu ambao siyo raia wanajiandikisha.
Aliongeza kuwa maombi ya hati za kusafiria yameongezeka maradufu kutoka hati 4,938 Julai 2014 hadi 8,703 Julai 2015 kwa upande wa Bara na kutoka hati 588 Julai 2014 hadi hati 1,028 Juni 2015 kwa upande wa Zanzibar.
Alisema idara inawataarifu wananchi kuwa siyo lazima kubadilisha hati inapokwisha muda wake, badala yake mmiliki anaweza kubadili na kupatiwa nyingine wakati wowote atakapokuwa akisafiri.
CREDIT: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment