Pages

Pages

Pages

Sunday 30 August 2015

KULALA MCHANA KUNAZUIA MSHTUKO WA MOYO


Uchunguzi unaonyesha kuwa kulala wakati wa mchana kunapunguza shinikizo la damu na pia kupunguza hatari ya kupatwa na mshutuko wa moyo pamoja na kiharusi.
Kulingana na utafiti, kulala kwa muda wa nusu saa ua zaidi wakati wa mchana hupunguza hatari ya kupatwa na mshutuko wa moyo kwa hadi asilimia 10.
Takriban watu 400 waliokuwa na shinikizo la damu walishiriki katika utafiti uliofanywa nchini Ugiriki. Matokeo ya utafiti huo yaliwasilishwa katika chama kinachohusika na masuala ya damu barani ulaya.
Watafiti sasa wanataka kufanya uchunguzi zaidi kuhusu matokeo yanayotakana na watu kulala saa za mchana.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment