Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 2 July 2015

TFF YATUMA SALAM ZA RAMBI RAMBI KWA MWAKELEBELA, MWAMBUSI

Frederick Mwakalebela

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Mwesigwa Selestine ametuma salamu za rambi rambi kwa famili aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela kufuatia kufiwa na baba yake mzazi jana mjini Irinnga na mazishi yakitarajiwa kufanyika kesho mjini Iringa.


Aidha TFF imetuma salam za rambi rambi kwa kocha mkuu wa timu ya Mbeya City, Juma Mwambusi kufutia kufiwa na mama yake mzazi mjini Mbeya.

TFF pia imetuma salam za rambi rambi kwa familia ya mtangazi maarufu wa wa michezo nchini Ezekiel Malongo  aliyefariki dunia jana.

Katika salam zake kwa familia ya Mwakalebela, Mwambusi na Malongo, Mwesigwa amesema wanawapa sana pole wafiwa kwa kuondokewa na wapendwa wao na kusema kwa niaba ya TFF, familia ya mpira na watanzania wote wapo nao pamoja katika kipindi hichi cha maombolezo.


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

No comments:

Post a Comment