Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 21 June 2015

CHELSEA, MAN CITY ZAMWINDA ALEX SONG

Alex Song (kulia)
Chelsea na Manchester City zimefanya mazungumzo ya kumsajili Alex Song kutoka Barcelona kulingana na mtandao wa Sky Sports.

Vilabu hivyo viwili hususan vinamtaka Song kwa kuwa anafuzu kuwa mchezaji wa nyumbani licha ya kuichezea Cameroon.
Song ambaye ameichezea West Ham msimu uliopita kwa mkopo ana miaka miwili ya kandarasi yake na Barcelona.
null
song
Hatahivyo West Ham ina matumaini ya kumsajili mchezaji huyo,lakini duru za Sky zinaamini kwamba kuna vilabu kadhaa vilivyo na hamu ya kununua ikiwemo City na Chelsea.
Mchezaji huyo wa miaka 27 ambaye aliichezea klabu ya Arsenal kwa miaka sita kabla ya kuelekea Barcelona miaka mitatu iliopita alicheza mechi 28 za West Ham msimu uliopita.
Barcelona iliomnunua mchezaji huyo kwa pauni milioni 15 inaaminika kutaka kumuuza mchezaji huyo kwa pauni milioni 5.
null
Song
Kandarasi yake katika klabu hiyo ya Nou Camp inaaminika kuwa ya kitita cha pauni 70,000 kwa wiki.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment