Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 21 June 2015

BANDA LA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI LAZIDI KUNG’ARA MAONESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA JIJINI DAR ES SALAAM

Displaying PIX 1 .JPG
Afisa Habari Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Rose Mdami (kulia) akitoa maelezo kwa mmoja wa wageni waliotembelea banda la Mamlaka hiyo kuhusu huduma zinazotolewa na Mamlaka hiyo, katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jjijini Dar es Salaam.
Displaying PIX 2 .JPG
Mwananchi aliyetembelea Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), akipewa maelezo na Afisa Habari Mkuu wa Mamlaka hiyo, Rose Mdami (kulia) kuhusu taarifa mbalimbali zinazoandaliwa na Mamlaka hiyo, katika maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja,jijini Dar es Salaam.
Displaying PIX 3 .JPG
Askari wa Jeshi la Polisi nchini,Tumaini Julius, akitoa maelezo kwa mwananchi aliyetembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na Jeshi hilo,  katika maonesho ya wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jjijini Dar es Salaam.
Displaying PIX 4 .JPG
Mmoja wa wananchi waliotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi akipiga picha  na  sanamu la askari linaloonyesha mavazi yaliyokuwa yanavaliwa  na askari wa kike, katika maonesho hayo ya Wiki ya Utumishi wa Umma  yanaendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja,jijini Dar es Salaam.
Displaying PIX 5 .JPG
Mkaguzi Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji, Dickson Rweza (kushoto), akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi waliotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika maonesho hayo ya Wiki ya Utumishi wa Umma  yanaendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment