Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 5 April 2015

KENYA KUOMBOLEZA KWA SIKU TATU

 
Rais Uhuru Kenyatta
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametangaza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kufuatia shambulizi la chuo kikuu cha Garissa ambapo takriban wanafunzi 148 waliuawa huku wengine 79 wakijeruhiwa.

Akihutubia taifa siku moja baada ya shambulizi hilo,rais Kenyatta amesema kuwa serikali yake itawachukulia hatua kali waliotekeleza shambulizi hilo.
Amasema kuwa waliopanga na kufadhili shambulizi hilo wako katika jamii na kwamba serikali itapata habari ya wahusika ili kukabiliana na wahalifu hao.
Amewataka wazazi,viongozi wa kidini pamoja na wale wa kisiasa kuchukua jukumu kufuatia vijana kupewa mafunzo ya itikadi kali na kwamba serikali yake haitakubali uongozi wa kidini kuanzishwa nchini Kenya na kuongezea kuwa atatea sera za kidemokrasia za taifa kwa gharama yoyote ile.
CREDIT: BBCSWAHILI

No comments:

Post a Comment