Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 24 March 2015

WANACHIMBA DHAHABU KUTOKA KWENYE KINYESI CHA BINADAMU

 
Amini usiamini wanasayansi nchini Marekani wameanza mikakati ya kusafisha dhahabu kutoka kwa kinyesi cha watu.

Kwa mujibu wa ripoti moja watafati hao wanasema kiwango cha dhahabu na madini mengine nadra na yenye thamani ya juu kwenye
vituo vya kusafishia kinyesi inazidi idadi ya utafiti unaofanywa katika katimbo nyingi za dhahabu.
''Kiwango cha dhahabu hapa ni cha juu zaidi ya viwango vinavyotumiwa na watafiti kubaini iwapo mgodi una madini hayo ya kutosha au la''
Ripoti hiyo imechapishwa katika kongamano la 249 la wanakemia wa Marekani '' American Chemical Society (ACS) iliyoandaliwa huko Denver Marekani .
Kulingana nao iwapo kutatambuliwa mbinu ya kusafisha kinyesi na kuitenga dhahabu atakayegundua mbinu hiyo ataisaidia sana mazingira.
Daktari Kathleen Smith, aliyesaidia katika uandishi wa ripoti hiyo kinyesi cha watu kina kiwango cha juu mno cha dhahabu, fedha ,palladium na vanadium.
'' madini hayo ya vanadium shaba yanamanufaa makubwa sana katika utengenezaji wa bidhaa zinazotumika katika simu za mkononi na kompyuta mbali na bidhaa mbalimbali za kielektroniki.

Kinyesi kutoka kwa wamarekani milioni moja inazaidi ya dhahabu na madini yenye thamani ya dola milioni 13.
Marekani huwa inasafisha zaidi ya tani milioni saba ya kinyesi kila mwaka kulingana na dakta Dr Smith.
Nusu ya uchafu huwa hutumika tena kutengeza mbolea katika misitu huku nusu iliyosalia ikitumika kurejesha ubora wa ardhi baada ya kuchimbwa kwa madini tofauti tofauti nchini humo.
Watafiti hao wanatumia mbinu maalumu inayotumia kemikali ifahamikayo kama '' leachates'' kufyonza madini kutoka kwenye mawe.
Utafiti huu unatilia pondo utafiti wa awali uliodai kuwa kinyesi kutoka kwa wamarekani milioni moja inazaidi ya dhahabu na madini yenye thamani ya dola milioni 13. CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment