Pages

Pages

Pages

Friday 13 March 2015

GAVANA WA KENYA ANUSURIKA KUUAWA NA AL SHABAAB



 
Gavana Ali Roba wa Kaunti ya Mandera

Mwanasiasa mmoja wa Kenya amenusurika shambulizi lililotekelezwa na kundi la Al shabaab.
Ali Roba ,ambaye ni gavana wa mji ulio mpakani wa Mandera alikuwa akisafiri kuelekea mjini humo wakati msafara wake ulipovamiwa.

Jaribio hilo sio la kwanza kuhusu maisha ya mwanasiasa huyo ambaye amekuwa akiongoza kampeni dhidi ya kundi hilo katika eneo hilo.
Wapiganaji hao tayari wamekiri kutekeleza shambulizi hilo na kusema wamefanikiwa kuwaua wanajeshi wanne,kuchoma magari mawili na kutoroka na jengine.
Kufikia sasa polisi wa Kenya hawajathibitisha matamshi hayo ya kundi hilo.

CHANZO: BBC

No comments:

Post a Comment