Kapteni Lowassa akipiga tizi mjini Dodoma
Na Emma Kaaya via Wanabidii
Edward Lowassa ndiye Waziri Mkuu aliyewai kukaa katika
kiti cha uwaziri mkuu kwa muda mfupi zaidi kuliko waziri mkuu yeyote
yule; sasa angalia hii rekodi yake ya kushangaza:
Mosi,
Ndani
ya muda mfupi sana alionyesha nia ya dhati kukabiliana na foleni ya
jiji la Dar, tatizo ambalo kimsingi ni kama jinamizi kwa sasa!!!!
Mbili,
Ndani
ya muda mfupi sana alionyesha kukabiliana na tatizo la ajira kwa
vijana. Pale bandarini kulikuwa na watu waliokuwa vibarua kwa muda wa
zaidi ya miaka 15 lakini alipoingia uwaziri mkuu, ile hali kaisimamia mpaka jamaa wale wakapata mikataba ya kudumu.
Tatu,
Ndani
ya muda mfupi alionyesha kujali elimu kwa wananchi. Hizi shule za kata
ambazo ndizo zinazosaidia wananchi kuamka kwa sasa ni matunda ya
Lowassa.
Nne,
Tatizo la mikopo kwa
wanafunzi wa elimu ya juu. Akiwa bungeni mara nyingi amekuwa akiongelea
suala hili la mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kiasi kwamba ilibaki
kidogo tu ingekuwa malalamiko ya mikopo kwa wanafunzi yangekuwa historia.
Tano,
Wakati
akiwa waziri mkuu, kwa muda mfupi sana ilionekana kuwa uchumi sasa
utapaa; na tayari kulikuwa na viashiria (indicators) vya kutosha katika hilo.
Sita,
Kwa muda mfupi sana utendaji serikalini ulikuwa unakwenda kwa kasi ya ajabu. Kuanzia mdogo hadi mkubwa.
Saba,
Kwa
muda aliokaa hajawahi hata mara moja kutoa kauli tata za kuashiria
ubabe kwa wale wanaopingana naye. Kauli zake siku zote zimekuwa very
straight kuwakabili watumishi wazembe na watendaji wanaotenda kazi
katika mfumo wa business as usual. Tazama alivyomwajibisha Mhandisi wa Manispaa ya Temeke mara baada ya ghorofa la Chang'ombe Village lilipoporomoka; Tazama alipoamua kuingilia katika mkataba wenye utata wa kampuni ya maji Dar, hakusubiri siasa zichukue nafasi, tofauti na sasa.
Nane,
Ndiye kiongozi pekee serikalini ambaye ana rekodi ya kutoa individual support
kwa mwananchi mmoja mmoja pale atakapobaini kuwa panahitajika support
kwa ajili ya huyo mwananchi. Hata BBC Swahili walishawahi kuripoti
kuhusu hili.
Tisa,
Akiwa waziri mkuu
alimbeba sana Kikwete kwenye utendaji wa kiserikali! Hadi sasa Kikwete
amekata tamaa kabisa na mambo ya serikali. Anatamani siku anarudi toka Maryland akute tayari 2015 imefika maana hana hamu kabisa na mwenendo wa
mambo ndani ta taifa hili.
Kumi,
Kikwete
hatakaa amsahau kwa kumpoteza katika utendaji wa serikali yake. Na ndiyo
maana uchaguzi wa 2010 Kikwete alipata shida sana! Na hadi leo anamlilia
sana, ila mfumo wa chama chake unamgandamiza sana.
HAYA SASA
Kuna waliokaa kwa muda mrefu ambao waliishia kuwaambia wafanyabiashara "...Ukitaka mambo yako yawe mazuri jiunge na CCM...!"
CREDIT: Kwa hisani ya Wanabidii ingawa imehaririwa na Moderator.
No comments:
Post a Comment