Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 18 October 2014

HAK'YANANI, MWAKANI TUNAMTAKA RAIS WA AINA HII!


Ndugu zangu,
Tunapoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 lazima tutafakari ni Rais gani ambaye atatufaa. Kwa maoni yangu, tunahitaji Rais anayewapa majukumu watendaji wake na kusimamia utekelezaji. Ambaye yuko tayari kuwajibika na kuwawajibisha watendaji wake pindi wanaposhindwa kuwajibika wenyewe.

Tanzania ili iendelee inahitaji Kiongozi shupavu kweli kweli asiye na masihara. Taifa lipo kwenye umaskini mkubwa, watu wanateseka bila sababu ya msingi.
Tunahitaji Rais Shupavu, Jasiri, Mthubutu, Mwenye kuweka malengo na kusimamia utekelezaji wake ili tuyafikie hayo ‘Matokeo Makubwa Sasa’ katika maeneo yote muhimu kuanzia kwenye elimu, uchumi, kilimo, ulinzi na usalama, na zaidi kurudisha uzalendo kwa wananchi.
Tunahitaji Rais anayeweka vipaumbele na kutambua namna tunavyoweza kufikia, siyo kwa kujaza makaratasi kwenye makabati.
Tunahitaji Rais asiyeyumba, ambaye upepo ukipuliza anapoteza mwelekeo. Lazima ahakikishe anakabiliana na mawimbi kwa manufaa ya umma.
Tunahitaji Rais ambaye ni dikteta kidogo na mwanadiplomasia kidogo ili mambo yaende. Mtu anayeweza kuchukua hatua mara moja mambo yanapokwenda kombo badala ya kusitasita.
Tunahitaji Rais msikilizahi, mfuatiliaji, asiye kigeugeu wala mvivu.
Tunahitaji viongozi ambao wanafuatilia utendaji, wanafanyia kazi taarifa na changamoto za wananchi na taifa kwa ujumla. Wanaoweza kuchukua hatua mapema kabla mambo hayajaharibika.
Tena basi hata watendaji wake wanapaswa kuwa wanamipango wenyewe badala ya kusubiri Rais awapangie.
Hakika, zama za 'kula bata' kwa mawaziri kwa kutumia kodi za walalahoi ziishe sasa kabla hatujaingia mwaka 2015, vinginevyo tutaanza kuwawajibisha hata mawaziri na wabunge mara watakapokuja kuomba kura zetu.
Hakuna binadamu aliyekamilika, lakini kwa hotuba hii - haijalishi Kiingereza chake kibovu kwa sababu siyo lugha yake ya asili - hakika Jenerali Iddi Amini hakuwa mbaya kiasi hicho, alikuwa dikteta lakini alipenda uwajibikaji na matokeo bora. Mnasema jamaa hakuwa msomi, kwa hotuba hii naamini huhitaji kuwa na lundo la shahada ndipo utambue kwamba Iddi Amini alikuwa anajali uwajibikaji kwa maslahi ya wananchi wote - siyo uzembe na kufumbiana macho!
Kwa hiyo, wale ambao wanaota ama kuoteshwa kugombea urais mwaka 2015, wangeoteshwa pia kama wano uwezo wa kuthubutu kufanya kama Jenerali Iddi Amini - kidikteta kidogo na kidemokrasia kidogo - kinyume chake taifa litazama!
Haya ni maoni yangu tu.

Ndugu yenu,
Daniel Mbega
0656-331974


No comments:

Post a Comment