Taarifa kwa Vyombo Vya
Habari, 30 Octoba 2014
Serikali isikwepe kulipa malimbikizo ya madeni MSD
kuokoa maisha ya Watanzania!
Sikika imesikitishwa na tamko lililotolewa na Waziri wa Afya na Ustawi
wa Jamii, kuhusiana na kushindwa kwa vituo vya huduma za afya kununua dawa MSD
kutokana na kuongezeka kwa deni. Ni wazi kuwa waziri hajalipa tatizo hili uzito
unaotakiwa na kutambua kuwa baadhi ya wagonjwa wanaweza kupoteza maisha
kutokana na tatizo hili.