Pages

Pages

Pages

Thursday 30 October 2014

CHAMA CHA NIDAA CHASHINDA TUNISIA

Kiongozi wa Nidaa Tounes
Chama cha kidini nchini Tunisia Nidaa Tounes kimeshinda viti 85 katika uchaguzi wa ubunge nchini humo kulingana na matokeo.

Chama tawala cha Ennahda kimejishindia viti 69 katika bunge hilo la viti 217.
Matokeo rasmi yamethibitisha ubashiri wa awali na maafisa Ennahda wametoa wito kwa chama cha Nidaa kubuni serikali ya umoja.
Serikali ya mpito iliobuniwa ili kurejesha demokrasi nchini Tunisia baada ya mapinduzi ya mwaka 2011 imeungwa mkono na wengi.
Wafuasi wa Nidaa
Nidaa Tounes kimepata viti 85 kati ya viti 270 vya ubunge. Ennahda kilijipatia viti 69.
Uchaguzi huo ulikua wa kwanza chini ya katiba mpya na waandishi wa habari wamesema ni hatua kubwa kwa Tunisia katika kuafikia mfumo wa demokrasia baada ya miongo ya utawala wa kiimla.
Takriban raia millioni tano wa Tunisia walisajiliwa kushiriki katika shughuli hiyo.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment