INNOCENT A. NDAYANSE
(ZAGALLO)
0755 040 520 / 0653 593
546
ILIPOISHIA:
Judith amefanikiwa
kubadilisha fedha na kurejea Magomeni ambapo anaamua kupata supu. Mara anatokea
Edson, kijana mtanashati na mwenye haiba ya kutosha ambaye anaomba kuketi
mezani. Wote wawili nyoyo zinasabahiana na Edson anafarijika zaidi anapoambiwa na
Judith kwamba hajaolewa. Huko Kigali, Rwanda Makella amechanganyikiwa baada ya
kukimbiwa na Judith. Anaamua kwenda kwa Jamilla mke wa Ramadhani, mwanajeshi
mwenzake, na anapofika anamkumbatia kwa nguvu mwanamke huyo ambaye anajitahidi
kujinasua bila mafanikio. Ramadhani anaposikia purukushani hizo na kumuona
Makella anaamua kutoka amua na bastola. Je, nini kitaendelea? Ungana na
msimulizi wako …
Makella akashtuka na kumwachia Jamillah. Akageuka na kukutana uso kwa
uso na Ramdhani aliyekuwa amemlenga kwa bastola. Makella akaduwaa. Akatamani
kutamka neno asiweze.
Akayashuhudia macho ya Ramadhani yakimtazama bila ya kupepesa na
yakitangaza jambo moja tu; NITAKUUA.
Mara akahisi kitu kikipenya kifuani, kikamzulia joto kali kisha maumivu
yakaanza kumwingia kwa mbali. Nguvu zikaanza kumomonyoka maungoni, Uwezo wa
macho kuona ukawa ukimkimbia kwa kasi ya kutisha. Miguu ikashindwa kuubeba
mwili. Akamwona Makella akigeuka na kurudi chumbani na bastola yake.
Cha mwisho alichoambulia ni yowe kali la Jamillah na alipoanguka
sakafuni hata maumivu hakuyasikia!
**********
MSHTUKO alioupata Judith pindi alipokutanisha macho na Edson haukuwa wa
kawaida. Na alikumbuka mara ya mwisho alipoupata mshtuko wa aina hiyo ni siku
alipokumbana na Zalidi, kijana ambaye alitokea kumvutia kwa kiasi kikubwa.
Zalidi naye alikuwa Mtutsi na waliishi wote mjini Kigali, Rwanda lakini wakiwa
mbalimbali kwa makazi.
Zalidi aliporusha ndoano, Judith alikosa uwezo wa kuikwepa. Akanaswa.
Wakawa wapenzi. Lakini kabla hawajafikia ile hatua ambayo Zalidi aliihitaji
sana, hatua ya kustarehe kimwili, mauaji yalitokea mtaani alikoishi Zalidi.
Wazazi wake Zalidi pamoja na Zalidi mwenyewe, waliuawa kikatili na askari wa
Kihutu.
Tangu hapo Judith hakujua kupenda wala kutamani hadi siku hii alipopata
tena mshtuko huu, mshtuko ulioifanya akili yake ivurugike kiasi cha kujikuta
akiwa mwepesi wa kujibu kuwa hajaolewa. Na ndipo maongezi kati yao yaliponoga,
Edson akiwa kinara.
Waliachana baada ya saa tatu, maongezi baina yao yakiwa yamewaweka
karibu zaidi.
Sasa Judith alijikuta akifungua ukurasa mpya. Akatamani kila wakati awe
na Edson. Hata aliporudi kule gesti, mawazo yake yote yalikuwa kwa Edson. Alikuwa
na hamu wawe pamoja, wakumbatiane na hatimaye kufanya kila kitu ambacho mioyo
yao ingewashawishi. Kwa ujumla alimpenda na kumhitaji Edson kwa kiwango
kikubwa. Ndipo akajiwa na wazo la
kumtoroka Baraki, mfadhili wake tangu Rwanda.
Alitambua fika kuwa, haitakuwa busara kumtoroka Baraki, lakini afanye
nini? Huyo Baraki mwenyewe ana mke. Vipi amtegemee mtu wa aina hiyo katika
maisha yake? Na pia, kiwango cha pesa alizokuwa nazo kilikuwa kichocheo kingine
katika kumfanya amtoroke Baraki.
Si tu kwamba kwa kuwa amekutana na Edson na kuvutiwa naye ndiyo maana
akaamua kumkimbia Baraki. La hasha. Alijua kuwa mapenzi ya Baraki hayatadumu,
ni mapenzi ya muda tu, mapenzi ambayo siku yatakapoyeyuka ndipo atakapojikuta katika dunia mpya, katika
maisha mapya.
Hivyo, hakutaka kupoteza muda. Jambo la kwanza aliloamua kulifanya ni
kuondoka katika gesti hiyo. Ndiyo, aondoke na kwenda kuishi popote. Kama ni
suala la pesa, hilo halikuwa tatizo. Pesa anazo, tena za kuweza kumlinda kwa
siku nyingi. Ni kipi kitakachoharibika? Hakuna.
Alipofika gesti tu, alitwaa kila kilicho chake na kuondoka huku
akimwambia yule mhudumu kuwa Baraki amemwagiza wakutane mtaa wa pili kwenye baa
moja anakopata bia.
“Ndiyo uondoke na mizigo?” mhudumu alimhoji kwa mshangao.
“Ameniagiza kuwa niende nayo,” Judith alijibu kisha akaongeza, “Kwani
kuna tatizo gani? Anadaiwa?”
“Hapana, nauliza tu shemeji yangu.”
Ni hapo mtoto wa kike, msichana mrembo, msichana wa Kitutsi, Judith
Ndayishimiye alipotokomea kisayansi. Usiku wa siku hiyo ukawa ni yeye na Edson,
Edson na yeye. Siku mbili baadaye walikutana tena, hatimaye ikawa haipiti siku
bila ya kuonana. Uhusiano wao ukazaa uchumba kamili. Na ni katika muungano huo
ndipo Judith alipoamua kumtobolea ukweli kuhusu historia ya maisha yake.
Ilikuwa ni hadithi iliyomsononesha sana Edson. Na akaahidi kuitunza siri
hiyo.
“Usihofu, Judith,” alimwambia. “Lakini nakuahidi kuwa hutapata shida
yoyote. Cha muhimu, ni wewe kujitahidi kutomropokea mtu yeyote kuhusu mkasa
huo. Pole sana, mpenzi. Hayo ni mapito tu. Huenda Mungu alipanga wewe usiuawe
na uje kuishi huku Tanzania. Uje kumwondolea upweke Edson.”
Mwaka mmoja baadaye, ndoa kati ya Judith na Edson ilifanyika. Sherehe
kubwa ikafuata. Watu wakala, watu wakanywa na kusaza.
**********
SIKU moja, ikiwa ni miaka mitatu baada ya Edson na Judith kufunga ndoa,
Judith alikuwa eneo la Kariakoo na mwanaye, Jerome ambaye wakati huo alikuwa na
umri wa mwaka mmoja na nusu. Alikwenda huko kutafuta nguo zake na za mwanaye
kwa ajili ya sikukuu ya Krismasi. Alipita mtaa huu na ule, akiingia duka hili
na lile, akiangalia nguo hii na ile.
Hatimaye, katika pitapita yake hiyo, aliingia katika duka moja Mtaa wa
Kongo. Duka hilo lilisheheni watu. Humo alitulia akiangalia kwa makini nguo
nyingi zilizokuwa katika mauzo. Kulikuwa na wahudumu wawili ambao
waliwasikiliza wateja huku mmiliki wa duka, mzee wa Kihindi akiwa ameketi
kitini, meza iliyosheheni makabrasha ikiwa mbele yake.
Judith alijisogezasogeza hadi mbele na kumgusa mhudumu mmoja huku
akimwambia, “Kaka, nipatie ile blauzi nyekundu.”
Itaendelea kesho…
ZILIZOPITA:
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 19
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 18
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 17
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 16
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 15
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 14
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 13
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 12
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 11
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 10
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 10
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 9
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 8
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 7
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 6
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 5
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 4
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 3
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 2
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 1
ZILIZOPITA:
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 19
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 18
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 17
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 16
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 15
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 14
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 13
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 12
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 11
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 10
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 10
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 9
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 8
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 7
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 6
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 5
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 4
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 3
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 2
RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 1
No comments:
Post a Comment