Kama igizo vile: Mlinda mlango wa Argentina Sergio Romero akiokoa mkwaju wa penati uliopigwa na Ron Vlaar.
KOCHA wa Uholanzi, Louis van Gaal amekiri kuwa wachezaji wawili waligoma kupiga penati ya kwanza baada ya kufungwa kwa penati na Argentina.
Uholanzi walishindwa kurudia kupiga penati kama walivyofanya katika hatua ya robo fainali dhidi ya Costa Rica baada ya beki wa Aston Villa Ron Vlaar kukosa penati ya kwanza na Wesley Sneijder naye kukosa.
Argentina walifunga penati zote nne na kufika fainali ya kombe la dunia ambapo watavaana na Ujerumani kwenye dimba la Maracana jumapili ya wiki hii.
Baadaye, Van Gaal – ambaye anatarajia kuanza kazi wiki ijayo katika klabu ya Manchester United - alijitokeza na kusema kuwa wachezaji wawili waligoma kupiga penati ya kwanza, lakini hakufafanua zaidi.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com
CHANZO FULL
SHANGWE
No comments:
Post a Comment