Pages

Pages

Pages

Tuesday 1 July 2014

FISI, NYOKA MKUBWA WAJISALIMISHA KWA WANANCHI


Na Mwandishi Wetu, brotherdanny5.blogspot

ARUSHA: KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida wananchi zaidi 300 wamelazimika kumuuua mnyama pori aina ya fisi pamoja na nyoka wa msituni ambaye alikuwa anafugwa kwa imani za kishirikina.
Aidha tukio hilo limetokea wiki iliyopita katika eneo la Kibaoni Kata ya Kingori ambapo wanyama hao walitoka ndanikwa mkazi mmmoja wa eneo hilo mara baada ya kufanyika kwa maombi yaliyowakuitanisha wakazi wa mji wa Kibaoni.
Akiongelea tukio hilo Nabii ambaye amesababisha wanayama hao kutoka ndani walipokuwa wanafugwa, nabii Felix Ole Mpoke alidai kuwa yeye alikuwa kwenye utaratibu wake wa kawaida wa maombi lakini wakati anaomba aliita wanawake kwa ajili ya maombezi kwani wanawake kwa sasa wanakabiliwa na changamoto nyingi sana ikiwemo suala zima la utandawazi.
Alisema, wakati wanawake hao wanakuja kuombewa ndipo familia moja(jinalinahifadhiwa)ilikuja kwa kuwa walikuwa wanasumbuliwa na matatizo ya muda mrefu hivyo waliitaji nguvu na msaada wa mungu zaidi.
Aliongeza kuwa wakati maombezi hayo yakiwa yanaendelea ghafla Fisi ambaye kawaida yake huishi porini alitoka ndani ya nyumba moja ambayo na kukimbia ovyo katika eneo ambalo mkutano wa injili ulikuwa unaendelea hali ambayo ilizua tafrani kubwa sana .
“Maombi yakiwa yanaendelea dhidi ya familia ile kilichotokea ni kuwa fisi alichomoka ndani na kuja katika eneo la mkutano ambalo tulikuwepo na watu kwa kweli wengi wao walikimbia na kuona kama kitu cha ajabu sana," aliongeza Felix.
Wakati huo huo alidai kuwa wakati fisi huyo akiwa anatembeatembea katika eneo hilo pia ghafla naye nyoka ambaye asili yake ni porini naye alitoka ndani humo huku akiwa anamfuta fisi huyo ambaye anasadikika kuwa alikuwa wanaishi pamoja bila familia kujua ingawaje alikuwa anamilikiwa na baba wa familia hiyo .
Alisema kuwa wananchi wenye hasira kali walilazimika kuhoji maswali familia hiyo ambapo utafiti uliweza kubaini kuwa mama pamoja na watoto wa familia hiyo walikuwa hawajui kinachoendelea juu ya  umiliki wa wanyama hao ambapo utafiti uliweza kubaini kuwa ilikuwamali ya baba wa familia ambaye muda mfupi alitoroka mahali ambapo hapajulikana mpaka sasa.
Alibainisha kuwa baada ya hapo watu walillazimika kumburuta fisi huyo ambaye alikuwa na nyoka mkubwa sana mpaka maeneo ya madhabahu ya kanisa hilo ambapo waliweza kuwacbhoma moto hadi kuteketea
Hataivyo wananchi walioweza kuongea nawaandishi wa habari ambao walidhuru maeneo hayo ya kibaoni walisema kuwa ushirikina ndio chanzo kikubwa cha maendeleo kufifia katika eneo hilo ingawa linakaribiana na uwanja wa ndege wa kimataifa(KIA)hivyo jitiada za kupambana na ushirikina zinahitajika zaidi.

No comments:

Post a Comment