Pages

Pages

Pages

Friday 11 July 2014

DR. MWINYI MGENI RASMI MAONYESHO YA SILAHA

mwinyi
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Hussein Mwinyi.
Na Mwandishi wetu
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dk  Hussein Mwinyi anatarajiwa kufungua maonyesho ya  kongamano la Majeshi ya Nchikavu Afrika ya Mashariki ambapo zaidi ya wataalamu 300 .
Kongamano hilo ambalo Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ndiye mshirika mkuu linatarajiwa kufanyika julai 15 na 16  mwaka huu katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam ambapo lengo kuu ni  kujadili changamoto zinazowakabili.
 Mkurugenzi wa kongamano hilo la majeshi ya Nchikavu Afrika ya Mashariki, Tracey  Lee Zurcher, alisema kuwa Kutokana na misukosuko ya kisiasa wanayokumbana nayo sasa kwa upande wa uharamia na vikosi vya waasi, serikali hizi zinatakiwa kuongeza kwa kasi uwezo wa ulinzi wa nchi kavu pamoja na uwezo wa misaada ya kibinadamu.
“Nchi za ukanda wa Afrika ya Mashariki zina shauku kubwa ya kujilinda, sio tu kwa kuwa na maarifa bali pia kuwa na zana ili kuimarisha miundombinu ya ulinzi wao,” alisema.
Zurcher alibainisha kwamba makongamano  waliyoyafanya  yameonyesha kuwa kuna haja ya kuwa na ubora wa hali ya juu kimikakati na kiufundi kwa pamoja katika ngazi za kikanda.
 Zurcher alieleza kuwa  mbali ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kutazamia  kununua zana za kivita  lakini pia wanajivunia kuyakaribisha majeshi na wawakilishi wa serikali kutoka nchi za Uganda, Kenya, Tanzania, Rwanda na Burundi ambao wataelezea masuala muhimu kuhusu ulinzi kwa upande wa nchi kavu na majini pamoja na usalama kwa ujumla.
Pamoja na mambo mengine  Zurcher alisema kuwa wataalamu wa masuala ya kijeshi kutoka nchi za Afrika ya Kusini, Malawi, Ethiopia, Msumbiji, na Zambia pia wamealikwa.
CHANZO MO BLOG

No comments:

Post a Comment