Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 25 June 2014

WAGOMBEA 2000 WAWANIA NAFASI 200 TU ZA UBUNGE LIBYA

Uchaguzi nchini Libya
Upigaji kura umeanza nchini Libya ambapo raia wanachagua bunge jipya.
Bunge hilo litachukua nafasi ya baraza la kitaifa ambalo limekuwa likikumbwa na migawanyiko ya kisiasa na kimawazo kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Wananchi wa Libya wanaendelea kupiga kura kuchagua wabunge wapya.Huu ni uchaguzi wa pili kufanyika nchini humo tangu kumalizika kwa mapigano yaliyomng'oa mamlakani aliyekuwa kiongozi wa mda mrefu Muamar Ghaddafi .
Wanatumaini kuwa huu utakua mwanzo mpya baada ya malumbano ya kisiasa yaliyoshuhudiwa tangu kuchaguliwa kwa bunge la kwanza mwaka 2012.
Inaelekea kuwa idadi ya wapigaji kura ni ndogo ikilinganishwa na idadi ya wapigaji kura waliosajiliwa.
Wagombea wapatao 2000 wanagombea nafasi 200 za ubunge.
Kutokana na hofu ya usalama idadi ya waangalizi wa kimataifa ni chache.
Eneo la mashariki la Libya limekuwa likikabiliwa na machafuko yanayoshukiwa kuchochewa na makundi ya wanamgambo.

Maafisa wa uchaguzi wanatarajia shuguli za upigaji kura kutatizwa katika baadhi ya miji.
BBC

No comments:

Post a Comment