Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday, 12 June 2014

KOMBE LA DUNIA 2014 LIMEUZWA BRAZIL, TIKETI ZOTE KWISHNEI


Uwanja wa Corinthians jijini Sao Paulo ambapo leo fainali za Kombe la Dunia zinafunguliwa rasmi kwa mchezo baina ya wenyeji Brazil na Croatia.

Na James Truman, brotherdanny5.blogspot

Sao Paulo, Brazil: FAINALI za Kombe la Dunia zinaanza rasmi leo nchini Brazil ambapo wenyeji wanafungua dimba na Croatia kwenye Uwanja wa Corinthians unaomeza mashabiki 65,000 mara moja.
Wachunguzi wa masuala ya soka wanasema fainali za mwaka huu zitakazovutia mashabiki zaidi ya milioni tatu ndizo zilizoweka rekodi ya pekee kuanzia maandalizi yake hadi mapato.
Rekodi hizo ni pamoja na zawadi ya Dola 35 milioni (takriban Shs. 57.8 biloni) kwa shirikisho ambalo timu yake itatwaa ubingwa, Dola 4 bilioni (Shs. 6.6 trilioni) zitakazotokana na matangazo ya biashara kwa FIFA, na Dola 14 bilioni (Shs. 23.1 trilioni) kama mapato kwa Brazil, yaani nchi mwandaaji.
Kwa ujumla, fainali hizi ni tayari zimekwishauzwa, kwa saabu tiketi zote milioni 3 zilizotengwa na FIFA kwa ajili ya mechi 64 zinaonekana zimekwisha tangu zilipoanza kuuzwa Oktoba 2013.
"Tumepata mafanikio ya kiuchumi,” Katibu Mkuu wa FIFA Jerome Valcke aliwahi kukaririwa akisema. “Kuna mafanikio makubwa sana katika mauzo ya tiketi, hatujawahi kuuza tiketi nyingi namna hii."
Lakini furaha ya FIFA iko tofauti na hali halisi nchini Brazil.
Walipa kodi ndio wanaokamuliwa zaidi, katika taifa lenye watu milioni 200 ambao gharama za vitu zimepanda zaidi ya maradufu kutokana na uenyeji wa fainali za mchezo huo wenye waumini wengi duniani.
Kiasi cha Dola 14 bilioni ni jumla ya fedha ambazo zimetumiwa na Brazil katika ujenzi na ukarabati waviwanja 12 vitakavyotumika kwa mashindano hayo, kuboresha miundombinu ya jiji na maeneo mengine ya kiserikali pamoja na kuhakikisha usalama wa timu zote 32 na watazamaji 600,000 watakaokwenda huko, ambao tayari wengi wamekwishawasili.
Matumizi hayo makubwa yamesababisha vurugu nchini Brazil, na ilianza kujionyesha Juni 2013 wakati wa Kombe la Mabara ambapo wananchi walilalamika kwamba hawana shule bora, hospitali zinazofaa huku serikali nayo ikituhumiwa kwa rushwa.
"Wakati Brazil ilipoomba uenyeji wa Kombe la Dunia ilikuwa na bajeti ya kufanya hayo," alisema Valcke.
Katika fainali hizi FIFA itatumia Dola 2 bilioni (Shs. 3.3 trilioni), ikiwa ni pamoja na gharama za kamati ya maandalizi.
Lakini hayo yote yataipita Brazil. Hata kama nchi hiyo mwenyeji itapata hundi ya ubingwa Julai 13, fedha zitakazosalia Dola 323 milioni katika fungu la zawadi la FIFA zitakwenda kwa mataifa mengine 31 yanayoshiriki.
Shirikisho la Soka la Brazil pia linapata fungu kutoka kwenye Dola 48 milioni za FIFA kwa maandalizi, na Dola 70 milioni zinakwenda kwenye klabu (karibu zote za Ulaya) za Ulaya ambazo wachezaji wake wanawakilisha nchi zao.
Zawadi ya Dola 35 milioni (Shs. 57.8 bilioni) kwa bingwa wa dunia ni chini ya asilimia moja ya mapato ya FIFA iliyoyapata katika kipindi cha miaka minne ya fainali hizi.
Watangazaji na wadhamini wanalipa sehemu kubwa ya Dola 4 bilioni ambazo FIFA inatakiwa kupata.
Mtandao wa televisheni wa Ulaya umelipa sehemu kubwa ya fedha hizo karibu Dola 1.7 bilioni ili kupata haki ya kutangaza fainali hizo.
Wadhamini sita wakuu — Adidas, Coca-Cola, Emirates, Hyundai, Sony, Visa — kwa pamoja wanalipa Dola 177.125 milioni kila mwaka. Hiyo ni karibu Dola 708.5 milioni kwa miaka minne.
Wadhamini nane wanaofuatia — Budweiser, Castrol, Continental, Johnson & Johnson, McDonald's, Moy Park, Oi, Yingli — kwa pamoja wanalipa Dola 524 milioni. Karibu Dola 120 milioni zimevunwa kutoka kwa watangazaji wa ndani wa Brazil, kwa mujibu wa ripoti za mapato za FIFA za mwaka 2011-13.
FIFA pia inapata mamia ya mailioni kutoka kwa mashabiki wanaonunua tiketi kwa ajili ya kuingia viwanjani, ikiwa ni pamoja na taasisi zinazonunua viti maalum vya hisani na bidhaa zinazouzwa humo.
Matangazo kadhaa nchini Brazil yanaonyesha kwamba mapato ya FIFA hayatozwi kodi hapa. Wadhamini wa Kombe la Dunia na vyombo vya habari navyo vimesamehewa kodi.
FIFA, hata hivyo, imewekeza sana Brazil. Iliipatia kamati ya maandalizi Dola 221.6 milioni, na Februari mwaka huu FIFA ililipia karibu Dola 20 milioni kwa ajili ya umeme wa majenereta kwa shughuli za matangazo.
Uwekezaji wa FIFA unahusisha makumi ya mamilioni kwa vituo vya TV.
Mwaka 2010 kule Afrika Kusini, mchezo wa fainali baina ya Hispania na Uholanzi ulitazamwa na watu 530.9 ulimwenguni kote. Zaidi ya watu milioni 900 wala walitazama dakika moja ya mchezo huo nyumbani, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa, na kwa ujumla upo uwekezano wa watu bilioni moja kutazama walau sehemu ya mchezo huo.
FIFA inatumia fedha nyingi katika soka, ambapo Dola 1.4 bilioni ni kwa ajili ya kulifanya shirikisho hilo liendeshe shughuli zake pale Zurich na kuandaa mashindano mbalimbali – yakiwemo Fainali za Kombe la Dunia la Wanawake, mashindano ya dunia ya vijana chini ya miaka 17 na 20, Olimpiki ya Kiangazi, na Kombe la Dunia la Klabu.
Asilimia 75 ya mapato ya FIFA yanazama kwenye soka, ikiwemo mgawo wa Dola 250,000 kila mwaka kwa nchi 209 wanachama wake. Mashirikisho sita ya mabara yanapata Dola 2.5 milioni kila moja, na Dola 25 milioni zilitumika mwaka 2013 kwa shughuli za maendeleo, ikiwemo ujenzi wa viwanja.

Gharama za maandalizi
Rekodi zinaonyesha kwamba, fainali za mwaka huu ndizo zilizogharimu fedha nyingi zaidi kuliko zilizopita.
Brazil, kama ilivyoelezwa hapo juu, imetumia Dola 14 bilioni kwa mwaandalizi ya mwaka huu, wakati ambapo katika fainali za 2010, Afrika Kusini ilitumia Dola 4 bilioni; fainali za 2006 Ujerumani ilitumia Dola 6 bilioni; fainali za 2002 Korea Kusini na Japan kwa pamoja zilitumia Dla 5 bilioni; fainali za 1998 Ufaransa ilitumia Dola 340 milioni; na fainali za 1994 Marekani ilitumia Dola 30 milioni, pengine kwa sababu viwanja vyake vingi vilikuwa na hadhi kubwa.

Zawadi
Jumla ya zawadi zitakazotolewa na FIFA kwenye mashindano hayo ni Dola 576 milioni (ikiwemo Dola 70 milioni kwa klabu zenye wachezaji wanaoshiriki), likiwa ni ongezeko la asilimia 37 kulinganisha na zilizotengwa kwenye fainali ya mwaka 2010.
Kabla ya mashindano, kila timu shiriki kati ya 32 ilipatiwa Dola 1.5 milioni (Shs. 2.5 bilioni) kwa ajili ya gharama za maandalizi.
Mchanganuo unaonyesha kwamba, kila timu itakayotolewa katika hatua ya makundi itakomba Dola 8 milioni (Shs. 13.2 bilioni) wakati timu itakayoishia hatua ya mtoano itapata Dola 9 milioni (Shs. 14.9 bilioni) huku ile itakayoishia robo fainali ikilamba Dola 14 milioni (23.1 bilioni).
Aidha, timu itakayoshika nafasi ya nne itapata Dola 20 milioni (Shs. 31.2 bilioni), mshindi wa tatu atapata Dola 22 milioni (Shs. 36.3 bilioni), mshindi wa pili Dola 25 milioni (Shs. 41.3 bilioni), na bingwa atanyakua Dola 35 milioni (Shs. 57.8 biloni).
Ni utajiri mtupu.
Endelea kufuatilia blog hii kwa habari mbalimbali…


No comments:

Post a Comment