Aliyekuwa kocha mkuu wa Yanga, Mholanzi Van der Pluijm (wa kwanza kulia) anatarajia kuungana na Mkwasa (wa pili kulia) nchini Saudi Arabia
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
KOCHA msaidizi wa klabu ya Yanga, Mtanzania Charles Boniface Mkwasa ametimkia Uarabuni kuungana na aliyekuwa bosi wake msimu uliopita Mholanzi, Hans Van Der Pluijm.
Pluijm baada ya kumaliza mkataba wake wa miezi sita Yanga, aliamua kuondoka kwenda Saudi Arabia kuifundisha klabu ya ligi kuu ya Saudi Arabia iitwayo Al Shoalah FC .
Kocha huyo Mholanzi aliondoka kwa makubaliano maalum na Yanga, huku akieleza kuwa wakati anajiunga na Yanga aliwaambia kuna dili anasubiria na kama litakwenda sawa ataondoka.
Baada ya mambo kwenda sawa, aliondoka Yanga na kuagana kwa amani na uongozi wa Yanga pamoja na wanachama.
Pluijm alionekana kumkubali Mkwasa na sasa ameamua kumtafutia kazi nchini Saudi Arabia na kocha huyo Mtanzania anakwea pipa usiku huu.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com
CHANZO FULL SHANGWE
No comments:
Post a Comment