Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday, 23 June 2014

KOCHA YANGA SC AMFUATA HANS VAN DER PLUIJM SAUDI ARABIA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_BNr03B5QRrKffOr075ABic2DUpYD32qeJGulpH8wOMPzHBKnrixzHEYOYAUY_UC9o-KrTKimdVrezi66mp7fpR8j29gCMnQTJvG0a9OLmazGA_c6iA26pcWLEP39un0AbfsJYh7R4dcN/s1600/DSC_0027.JPG
Aliyekuwa kocha mkuu wa Yanga, Mholanzi Van der Pluijm (wa kwanza kulia) anatarajia kuungana na Mkwasa (wa pili kulia) nchini Saudi Arabia
 
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
KOCHA msaidizi wa klabu ya Yanga, Mtanzania Charles Boniface Mkwasa ametimkia Uarabuni kuungana na aliyekuwa bosi wake msimu uliopita Mholanzi, Hans Van Der Pluijm.
Pluijm baada ya kumaliza mkataba wake wa miezi sita Yanga, aliamua kuondoka kwenda Saudi Arabia kuifundisha klabu ya ligi kuu ya Saudi Arabia iitwayo Al Shoalah FC .
Kocha huyo Mholanzi aliondoka kwa makubaliano maalum na Yanga, huku akieleza kuwa wakati anajiunga na Yanga aliwaambia kuna dili anasubiria na kama litakwenda sawa ataondoka.
Baada ya mambo kwenda sawa, aliondoka Yanga na kuagana kwa amani na uongozi wa Yanga pamoja na wanachama.
Pluijm alionekana kumkubali Mkwasa na sasa ameamua kumtafutia kazi nchini Saudi Arabia na kocha huyo Mtanzania anakwea pipa usiku huu.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com

CHANZO FULL SHANGWE

No comments:

Post a Comment