Nimeitazama sana shoo hii nikavutiwa nayo. Aliyeitengeneza ninampa heko kwa ubunifu huu maridhawa.
Kwa kweli, kama bendi zetu zote pamoja na wasanii wangekuwa wabunifu namna hii, hakika wangeweza kufanya kazi bora.
Siyo kwamba bendi zetu hazina shoo nzuri, la hasha. Lakini ikiwa shoo ya vikaragosi kama hii imependeza namna hii, naamini binadamu wanaweza kufanya zaidi ya hapa.
Nawasihi wasanii wetu pamoja na bendi zote kuumiza vichwa vyao na kutengeneza shoo kabambe ambazo zitaboresha kazi zao daima.
Ndugu yenu,
Daniel Mbega
Iringa, Tanzania
0656-331974
No comments:
Post a Comment