Mama wa mapcha hawa
amesema mapacha wake ni zawadi kubwa kwake
Mama mmoja nchini
Marekani, amejifungua mapacha waliozaliwa wakiwa wameshikana mikono.
Watoto hao pia
walikuwa wanapumua bila usaidizi wowote walipotolewa kutoka katika mashine
yenye hewa ya Oxygen.
Mama wa watoto hao,
alisema kuwa watoto hao waliopewa majina ya Jillian na Jenna Thistlewaite
walikuwa wameshikana katika kitovu na kutumia Kondo la nyuma moja , hali ambayo
madaktari walisema ni ya kipekee.
"Tayari ni
marafiki ,’’ alisema mama yao Sarah Thistlethwaite.
Walizaliwa Ijumaa
katika jimbo la Ohio, wakiwa wameshikana mikono.
Inaarifiwa ni mama
mmoja tu kati ya akina mama elfu kumi mwenye uwezo wa kujifungua mapacha wa
aina hiyo.
Bi Thistlewaite,
mwenye umri wa miaka 32,alilazimika kupumzika kwa wiki kadhaa kabla ya kujifungua
kwani mapacha wanaozaliwa wakiwa wameshikana mikoni ni hali nadra ambayo
inaweza kuhatarisha maisha ya watoto hao kabla ya kuzaliwa.
Mama huyo alisema
kupokea watoto wake ilikuwa zawadi tosha kwake wakati huu wa kusherehekea siku
ya akina mama duniani.
CHANZO, BBC
SWAHILI
No comments:
Post a Comment