Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 5 February 2014

ZAIDI YA KILO 200 ZA DAWA ZA KULEVYA ZAKAMATWA BAHARI YA HINDI

Jahazi lililokamatwa na madawa ya kulevya.
ZAIDI ya kilo 200 za dawa za kulevya aina ya Heroin yamekamatwa na kikosi cha polisi wanamaji katika Bahari ya Hindi yakisafirishwa kutokea nchini Irani pamoja na mabaharia kumi na wawili kutoka nchi ya Irani na Pakistani.
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Wanamaji Mboje Kanga ameeleza kuwa tukio hilo lililotokea usiku wa tarehe 4 majira ya saa sita usiku ambapo waliweza kukamata jahazi hilo na mabaharia kumi na mbili wote wakiwa hawaijui lugha ya Kiswahili wala Kingereza na jahazi lao halikuwa na utambulisho wowote wa sheria za majini.
Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa amesema jahazi hilo liliweza kukamatwa baada ya kikosi cha polisi cha wanamaji kuendelea na operesheni zake za doria majini na mara baada ya kulitilia shaka waliweza kulikamata na baada ya kulikagua walikamata shehena hiyo ya madawa ya kulevya aliyoyataja kuwa ni aina ya Heroin ambayo mengi huzalishwa nchini.
Chanzo: ITV

No comments:

Post a Comment