Akitoa taarifa hiyo leo mbele ya wanahabari Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma alisema kuwa miongoni mwa mafanikio makubwa ambayo mkoa wa Iringa unajivunia
ni katika sekta ya elimu, miundo mbinu, kilimo, afya na nyingine
nyingi.
Kwani alisema kuwa mkoa umepiga hatua katika ujenzi wa nyumba za walimu katika Halmashauri zote za Mkoa wa Iringa, lengo likiwa kuendelea kuboresha kiwango cha elimu katika mkoa.
Akielezea kuhusu sekta ya afya alisema kuwa hadi sasa hospitali
mbili zinaendelea kujengwa katika Manispaa na Kilolo, pia vituo vya
afya na nyumba za watumishi wa afya ikiwa ni pamoja na kuendelea
kusambaza dawa katika vituo vya afya.
Mkuu huyo wa mkoa alisema pia kumekuwepo na ufuatiliaji wa huduma zinazotolewa katika vituo hivyo na hospitali.
CHANZO: matukiodaima.com
No comments:
Post a Comment