MAHAKAMA
ya Mwanzo Namanyere wilayani Nkasi, Mkoa wa Rukwa imeingia kwenye
lawama kwa kitendo cha kuvunja ndoa iliyokuwa na mgogoro bila kugawanya
mali iliyochumwa kipindi cha wanandoa wakiishi kama mke na mume.
Bi.
Maria Tarafa (25) mkazi wa Kijiji cha Isale ambaye ni mmoja wa wanandoa
hao ametoa malalamiko hayo hivi mjini hapa alipokuwa akizungumza na
mwandishi wa habari hizi, huku akiituhumu mahakama hiyo haijampa nafasi
ya kujitetea kama akiwa kama mlalamikiwa.
Alisema mumewe, Ndebile Kazuri (31) alikuwa akitaka kumtelekeza yeye na watoto wao wanne kwa muda mrefu kwa kutaka kuivunja ndoa yao halali kinyemela, lakini alikuwa akimshinda kila alipoitisha vikao vya wazazi na viongozi wa vijiji na kata akitaka kuivunja ndoa hiyo bila kutoa haki kwa mama na watoto (huduma).
Alisema mumewe, Ndebile Kazuri (31) alikuwa akitaka kumtelekeza yeye na watoto wao wanne kwa muda mrefu kwa kutaka kuivunja ndoa yao halali kinyemela, lakini alikuwa akimshinda kila alipoitisha vikao vya wazazi na viongozi wa vijiji na kata akitaka kuivunja ndoa hiyo bila kutoa haki kwa mama na watoto (huduma).
Alisema
mume huyo wameishi naye kama mtu na mke wake tangu mwaka 2003 na
kufanikiwa kupata watoto wanne ambao walikuwa wakiishi eneo moja na baba
yao huku Kazuri naye akiishi na mwanamke mwingine eneo hilo ambaye pia
wamezaa naye.
“…Licha
ya kuishi naye amekuwa akinipiga na kunifukuza niondoke kwake na watoto
wangu nirudi kwetu, lakini mimi nimekataa mara zote na kumwambia
nitakuwa tayari kuondoka baada ya kupata haki zangu na watoto
kuhakikisha wako katika malezi mazuri,” alisema Bi. Tarafa.
Alisema
mumewe aliamua kwenda baraza la kata na kuomba barua ili aende
mahakamani kuiomba mahakama ivunje ndoa yake na mkewe aondoke na kurudi
kwa wazazi wake. Kazuri alifungua kesi katika Mahakama ya Mwanzo,
Namanyere Wilaya ya Nkasi Oktoba 28, 2013, kesi namba 26/2013
iliyosikilizwa na Hakimu aliyetajwa kwa jina la B. Stanley.
Alisema mahakama ilimwita kwa mara ya kwanza na kumsomea
maelezo ya mdai (mumewe) ya kuomba ndoa yao ivunjwe yeye alipinga na
kutaka awasilishe maelezo yake lakini mahakama iligoma kwa madai
ilichoitaji kwa mlalamikiwa ni kujibu kama yupo tayari au la na si
kupata maelezo.
“…Niliomba
niliomba nipewe nafasi ya kuzungumza upande wangu lakini walikataa na
kuniambia; mama tumekuja kusikiliza kesi ya talaka na si maelezo
mengine, we sema kama upo tayari au la…,” alisema.
Aliongeza
kuwa Novemba 18, 2013 baada ya yeye kukiri kuwa yupo tayari kuachana na
mume huyo iwapo atapata haki zake na watoto, mahakama ilivunja ndoa
hiyo na kuamuru aondoke na watoto wawili bila kueleza namna watakavyo
pata huduma toka kwa baba yao.
Alisema
mahakama iliamuru watoto wa miaka 7 na 9 watabaki kwa baba yao nay eye
kuondoka na wawili wenye miaka miaka chini ya saba. Aliongeza kuwa
Mahakama iliamuru apewe magunia 9 ya mahindi kati ya 10 ambayo tulilima
pamoja na bati 7.
“…Mume
wangu alidanganya kuwa hatuna mali pale mahakamani, mimi nikaeleza ni
uongo kwani tuna ng’ombe zaidi ya 127, buzi 30, nyumba mbili pale
kijijini Isale pamoja na hekari zaidi ya 70 za ardhi…hawakunisikiliza
pale mahakamani. Ukweli ni kwamba tunamali hizo ambazo tulichuma tukiwa
wote,” alisema Bi. Tarafa.
Mwandishi
wa habari hii amebahatika kupata nakala ya hukumu ya kesi hiyo, ambayo
kweli haikuonesha namna watoto wanaobaki kwa mama watahudumiwaje licha
ya kuamuru kuwa watabaki na mamayao.
Akizungumzia sakata hilo, Hakimu
Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya, Ramadhan Rugemalira alisema mama
huyo anahaki ya kufungua kesi ya madai kuomba mgawanyo wa mali na
matunzo kwa watoto endapo hakuridhika na hukumu iliyotolewa kwa shauri
hilo.
“…Anachotakiwa
kuomba mahakamani kwa sasa ni mgawanyo wa mali, kwamba katika kesi yao
ambayo mahakama ilivunja kuna mali ambazo mahakama haikuzizungumzia
kabisaa lakini na mimi (mke) ninahaki na mali hizo, unaona…ataleta
ushahidi kama ng’ombe hao wapo kama kuna ardà na nini…hivyo huyo
mwanaume ataitwa na kesi kusikilizwa,” alisema Rugemalira.
Hata
hivyo, Hakimu Rugemalira alisema huenda mtoa hukumu wa mwanzo aliteleza
kwa kitendo cha kutoainisha namna watoto wanaobaki kwa mama watalelewa
vipi.
Alisema pamoja na hayo bado mama huyo anahaki ya kufungua madai mengine kudai haki hizo.
Tulipozungumza na Kazuri juu la mali ambazo mke anazilalamikia, yaani ng’ombe
127, nyumba 2, mbuzi 30 na ardhi hekari 70 alisema mali hizo alipewa
na babayake wakati anaanza maisha hivyo bado ni mali ya babayake ambaye
alidai yupo hadi sasa.
Uchunguzi
uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini baba yake na Kazuri
(yaani Kazuri Moshi) ni marehemu alifariki tangu Machi 2004 na mali zake
kugawiwa kwa watoto wake.
Hata
hivyo mtalaka wake Kazuri anasema walipewa ng’ombe za urithi toka kwa
baba yake na Kazuri zikiwa 65 lakini wamezizalisha hadi kufikia idadi
zilipo sasa pamoja na mashamba na nyumba lakini anashangaa mzazi
mwenzake anamdhulumu kila kitu.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com kwa ushirikiano na TAMWA
No comments:
Post a Comment