Pages

Pages

Pages

Saturday, 8 November 2014

OBAMA AMTEUA LORETTA KUWA MWANASHERIA MKUU WA KWANZA MWANAMKE MWEUSI!

Loretta Lynch ateuliwa kuwa mwanasheria mkuu nchini Marekani
Ikulu ya White House nchini Marekani inasema kuwa Rais Brack Obama amemteua mwendesha mashtaka wa mji wa New York, Loretta Lynch, kuwa Mwanasheria Mkuu nchini humo.

Msemaji wa Ikulu ya White House alisema kuwa mkuu huyo mpya wa sheria atateuliwa rasmi leo Jumamosi.
Ikiwa uteuzi wake utaidhinishwa na Bunge la Seneti, Loretta Lynch, atakuwa mwanamke wa kwanza mwenye asili ya Afrika kuwa mkuu wa sheria nchini Marekani.
Uteuzi huo unafanyika wiki sita baada ya kujiuzulu kwa Eric Holder ambaye ndiye Mmarekani wa kwanza mweusi kuteuliwa kuwa mkuu wa sheria nchini humo.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment