Pages

Pages

Pages

Monday 5 December 2016

MATUKIO YA UHAKIKI WA WASTAAFU WANAOLIPWA NA HAZINA MKOANI ARUSHA

Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Msaidizi Bw. Stanslaus Mpembe (kushoto)  akitoa ufafanuzi kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango namna zoezi zima la uhakiki wa wastaafu kanda ya kaskazini linavyokwenda kabla ya uzinduzi wa zoezi hilo. Zoezi hili ni kwa mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga. 

Zoezi la kuhakiki wastaafu likiendelea katika Ofisi za Makao Makuu, Halmashauri ya jiji la Arusha, Pichani ni baadhi ya wastaafu wakifanyiwa uhakiki.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Doroth Mwanyika akiongea na baadhi ya wastaafu waliofika katika Ofisi za Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa ajili ya uhakiki ambapo wastaafu hao wameiomba serikali iwaongezee kiwango cha pensheni wanacholipwa ili waweze kukabiliana na hali ngumu ya maisha.
Mstaafu, Mwanakombo Yusuph, mkazi wa eneo la Kaloleni, Jijini Arusha, akihojiwa na Wanahabari mara baada ya kuhakikiwa katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha ambapo ameipongeza Serikali kwa kuendesha uhakiki huo utakaosaidia kuhuisha daftari la wastaafu na kwa uamuzi wake wa kuwalipa wastaafu kila mwezi badala ya miezi mitatu mitatu.

No comments:

Post a Comment