Pages

Pages

Pages

Sunday 2 October 2016

WANAFUNZI WA IHUNGO NA NYAKATO WAANZA KUWASILI WALIPOPANGIWA

 Mkuu wa Wilaya ya Bukoba (DC) Deodatus Kinawiro (wa kwanza kushoto) akitembelea maeneo mbalimbali katika Chuo cha Ualimu cha Bukoba kinachomikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (BLTC) kinachomolikiwa na Dayosisi ya Kaskazini Magharibi ambapo wanafunzi wa kidato cha tano kutoka shule ya sekondari Ihungo wataenda kusoma wakati shule yao inajengwa upya baada ya kuharibiwa kwa tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, mwaka huu. Wa kwanza kulia ni Mkufunzi katika chuo hicho Dafroza Protas.

Mkuu wa Wilaya ya Bukoba (DC) Deodatus Kinawiro (wa kwanza kushoto) akitembelea maeneo mbalimbali katika Chuo cha Ualimu cha Bukoba kinachomikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (BLTC) kinachomolikiwa na Dayosisi ya Kaskazini Magharibi ambapo wanafunzi wa kidato cha tano kutoka shule ya sekondari Ihungo wataenda kusoma wakati shule yao inajengwa upya baada ya kuharibiwa kwa tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, mwaka huu. Wa kwanza kulia ni Mkufunzi katika chuo hicho Dafroza Protas.
Mkuu wa Wilaya ya Bukoba (DC) Deodatus Kinawiro (wa pili kushoto) akikagua moja ya matanki ya kuhifadhia maji katika Chuo cha Ualimu cha Bukoba kinachomikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (BLTC) cha Dayosisi ya Kaskazini Magharibi ambapo wanafunzi wa kidato cha tano kutoka shule ya sekondari Ihungo wamehamishiwa kusoma wakati shule yao inajengwa upya baada ya kuharibiwa kwa tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, mwaka huu. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bukoba Mwantum Dau.
06. Muonekano wa baadhi ya majengo yatakayotumiwa na wanafunzi wa kidato cha tano kutoka shule ya sekondari Ihungo wataenda kusoma wakati shule yao inajengwa upya baada ya kuharibiwa kwa tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, mwaka huu.
(Picha na Eleuteri Mangi, MAELEZO, Bukoba)

Na Eleuteri Mangi, MAELEZO, Bukoba
Serikali imesema shule wanapohamishiwa wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita baada ya shule za sekondari za Ihungo na Nyakato kuharibiwa na tetemeko la ardhi kuharibu miundombinu ya shule hizo Septemba 10 mwaka huu.
Akizungumzia miundombinu ya Chuo cha Ualimu cha Bukoba kinachomikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (BLTC) kinachomolikiwa na Dayosisi ya Kaskazini Magharibi alipotembelea chuoni hapo, Mkuu wa Wilaya ya Bukoba (DC) Deodatus Kinawiro amesema kuwa mazingira wanapohamishiwa wanafunzi wa kidato cha tano kutoka shule ya sekondari Ihungo ni mazuri kwa kusomea yatawasaidia kupata elimu kama walivyokuwa kwenye shule yao ya Ihungo.
“Mazingira ya chuo ni mazuri sana, Serikali inaendelea kufanya marekebisho madogo madogo maeneo mbalimbali ya chuo ikiwa ni pamoja na miundombinu ya maji ili wanafunzi waendelee na masomo bila adha yeyote itakayowakwamisha kupata elimu” alisema  DC Kinawiro.
DC Kinawiro ameongeza kuwa Serikali imechukua hatua za haraka za kunusuru athari ambazo zingeweza kuwapata wanafunzi ambao shule zao zimeathirika zaidi kwa tetemeko la ardhi ambapo imelazimu kuwahamishia wanafunzi hao shule nyingi huku shule zao za awali za Ihungo na Nyakato zikiwendelea kujengwa upya.
Kuhusu kuwasili wanafunzi wa kidato cha tano katika chuo cha  ualimu cha BLTC mwishoni mwa wiki hii, Mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa walimu na wanafunzi hao wafike kwa wakati ili kuendelea na ratiba ya masomo bila kuchelewa hatua ambayo haitaathiri mtiririko wa kujifunza na kufundisha.
Akizungumzia mgawanyo wa wanafunzi wa shule za Ihungo na Nyakato, Afisa Elimu wa Mkoa wa Kagera Aloyce Kamamba amesema kuwa shule wanapohamishiwa wanafunzi wa shule hizo mbili zipo tayari kuwapokea wanafunzi hao na walimu wao ili waendelee na masomo.
Kuhusu mgawanyo wa wanafunzi katika shule walizopangiwa, Afisa Elimu Kamamba amesema kuwa wanafunzi wote wa kidato cha sita katika shule za Ihungo na Nyakato wamehamishiwa katika shule ya sekondari ya Omumwani ambapo wataendelea na masomo yao.
Shule hiyo ipo manispaa ya Bukoba mjini na miundombinu ya shule hiyo inaruhusu wanafunzi wa kidato cha sita kuendelea na ikizingatiwa wapo darasa la mtihani wa taifa ambao kwao ni muda wa maandalizi ya mitihani pamoja na kusoma kwa vitendo.
Kwa upande wa wanafunzi wa kidato cha tano kutoka shule ya sekondari Nyakato, Afisa Elimu Kamamba amesema kuwa wanafunzi wanaosoma tahasusi ya PCM ambao idadi yao ni 75 wamehamishiwa katika shule ya sekondari Kahororo, PGM wanafunzi 65 wamehamishiwa shule ya sekondari Biharamulo,  CBG wanafunzi 95 wamehamishiwa shule ya sekondari Nyailigamba, HKL wanafunzi 30 wamehamishiwa shule ya sekondari Kishoju, HGK wanafunzi 30 wamehamishiwa shule ya sekondari Nyakahura na HGE wanafunzi 45 wamehamishiwa shule ya sekondari Nyakahura.
Aidha, Afisa Elimu amewataka walimu na wanafunzi kitunza miundombinu ya shule wanazohamishiwa ili iendelee kuwasaidia wanafunzi katika kizazi cha sasa na kizazi kijacho na kuwahimiza walimu kutimiza wajibu wao wa kuwalea wanafunzi kitaaluma na kijamii kwa kuwa hiyo ndio kazi waliosomea.

  

No comments:

Post a Comment