Na Daniel Mbega
ULE Umoja wa
Katiba ya Wananchi (Ukawa) ulizikwa rasmi Machi 22, 2016 pale Karimjee wakati
Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta) umeporomoka kabla hata ya
kuusimamisha, hivi ndivyo ninavyoweza kusema.
Wakati
ambapo Ukawa umekufa baada ya kutimiza miaka miwili kamili, Ukuta umeporomoka
kabla ya kujengwa katika kipindi cha mwezi mmoja na nusu – kuanzia Julai 27
hadi Agosti 31, 2016.
Ukawa
ulianzishwa rasmi Aprili 16, 2014 baada ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba
kutoka vyama vinne vya upinzani – Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD – kususia
vikao kwa madai kwamba kulikuwa na mpango wa kuichakachua Rasimu ya Pili ya
Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambayo iliongozwa na Jaji
mstaafu Joseph Warioba.
SOMA ZAIDI
SOMA ZAIDI
No comments:
Post a Comment