Pages

Pages

Pages

Sunday 21 August 2016

SIMBA IMEANZA LIGI KUU NA MOTO WA DIZELI AU MABUA?


Mchezaji wa Simba Fredrick Magnon akiruka juu na golikipa wa Ndanda FC Jackson Chove huku wachezaji wa timu hiyo wakiangalia wakati mchezo huo wa Ligi Kuu ukiendelea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi, Agosti 20, 2016. Simba ilishinda 3-1.
 

SIMBA SC imeanza kwa kuongoza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kufuatia ushindi wake mkubwa wa mabao 3-1 dhidi ya Ndanda FC ya Mtwara katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Jumamosi, Agosti 20, 2016.

Kasi ya mchezo huo ilikuwa nzuri kwa Simba, ambayo mashabiki wa timu hiyo wanahoji iwapo itaendelea hivyo hivyo na kurejea kwenye ufalme wake au itakuwa kama moto wa mabua unaozima punde.

No comments:

Post a Comment