Pages

Pages

Pages

Monday 13 June 2016

MTANANGE MKALI WA TIMU YA BUNGE NA ALBINO DODOMA

 Mbunge wa Jimbo la Kalenga,ambaye ni mchezaji wa timu ya Bunge, Godfrey Mgimwa (kulia) akijiandaa kuwatoka wachezaji wa timu ya Albino katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma jana.Kutoka kushoto ni Dadi Kabe, Kelvin Mbuta na Ludovick Julius. Bunge ilishinda bao 1-0. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Mbunge wa Mkuranga wa timu ya Bunge, Abdala Ulega akiwania mpira na Kelvin Mbuta wa timu ya Albino

 Mbunge wa Jimbo la Kilolo, ambaye ni mchezaji wa timu ya Bunge, Venance Mwamoto (kulia), akimkaba mchezaji wa timu ya Albino, Kelvin Mbuta katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma
 Mbunge wa Jimbo la Kilolo, ambaye ni mchezaji wa timu ya Bunge, Venance Mwamoto (kulia), akimtoka mchezaji wa timu ya Albino, Kelvin Mbuta katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma
 Mwamoto akiwatoka wachezaji wa Albino

Mbunge wa Mbinga Mjini, Sixtus Mapunda  (kulia)akitafuta mbinu za kuwatoka wachezaji wa timu ya Albino

 Ludovick Julius wa Albino akiwahadaa wachezaji wa Bunge, Sixtus Mapunda na Godfrey Mgimwa

 Mgimwa akiwa amenyang'anya mpira

 Yusufu Kaiza akiwatoka wachezaji wa timu ya Albino


No comments:

Post a Comment