Pages

Pages

Pages

Monday 22 February 2016

TFF YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI FAMILIA YA MOSHA


hirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetuma salamu za rambirambi kwa familia ya mwandishi wa habari za michezo Fred Mosha kilichotokea jana alfajiri katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es salaam.
Katika salamu hizo, TFF imewapa pole familia ya marehemu, ndugu jamaa na marafiki kufuatia kifo hicho, na kusema wapo pamoja nao katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Fred Mosha mpaka umauti unamfika, alikuwa mkuu wa kitengo cha habari cha Tv/Redio Tumaini iliyopo jiini Dar es salaam na msiba upo nyumbani kwa marehemu eneo la Mbagala Saku kwa Mkongo.
Mazishi yanatarajiwa kufayika leo Jumatatu saa 9 mchana katika makaburi ya Kinondoni.

No comments:

Post a Comment