Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 6 October 2015

MAJENGO YA MKANDARASI KUGEUZWA CHUO CHA UFUNDI VETA


Na Mwandishi Wetu, NzegaMGOMBEA  Ubunge  kwa tiketi CCM  jimbo la Nzega Mjini Hussein Mohamed Bashe  amesema akichaguliwa mbunge wa jimbo hilo atahakikisha  majengo ya  kampuni ya Chinese Construction Company Limited (CCC) ya ujenzi wa barabara  kwa kiwango cha lami kutoka  Nzega  hadi Puge yanakuwa chuo cha ufundi stadi Veta.

Bashe  akiwahutubia wananchi wa mtaa wa majengo alisema kutokana na vijana wengi kushindwa kuendelea na masomo  kwa sababu mbalimbali majengo  hayo yatageuzwa matumizi kuwa chuo cha Veta kitakachoweza kusaidia  vijana ambao wangeweza kujiunga na makundi ya uhalifu.
Bashe alisema kuwa fursa hiyo itatokana baada ya wananchi kumchagua kuwa mbunge wa jimbo hilo la Nzega mjini  iliaweze kuwatumikia wananchi.
Alisema kuwa Mgombea  Urais  wa chama hicho John  Magufuli alimwambia wakati alipopita katika ziara yake na kupewa ahadi  ya suala hilo kuwa endapo atakuwa rais wa jamuhuri ya muungano ambi hilo litafanyiwa kazi na wananchi kunufaika na majengo hayo kwa kupata chuo cha VETA.
Alisema katika sula la kupata chuo cha VETA  anakila sababu ya kufanya jitihada kutokana na kundi kubwa la vijana kukosa ajira na badala yake kujikita katika matumizi ya madawa ya kulevya hali ambayo ni madhara kwa afya zao na familia kwa ujumla.
Kwa upande  wake mgombea  udiwani  wa kata ya Nzega mashariki  Elface Luangisa alisema changamoto  mbalimbali za kata hiyo anazifamu ikiwa na ukosefu wa kituo cha afya ambapo kwa sasa wananchi hupata shida kupata huduma za afya katika eneo  hilo.
Aliwataka ilikupata maendeleo ya uhakika bila matatizo wananchi wanapaswa kuchagua  mbunge wa ccm,diwani wa ccm pamoja na rais.

No comments:

Post a Comment