Pages

Pages

Pages

Tuesday 1 September 2015

WACHIMBAJI 2,500 WAHOFIA KUTIMULIWA BAADA YA UCHAGUZI


Wachimbaji wadogo

Na Hastin Liumba, Nzega
ZAIDI  ya wachimbaji  wadogo  2,500 katika mgodi mdogo wa dhahabu  wa Mwanshina uliopo wilayani  Nzega Mkoani Tabora wamehofia kufukuzwa mara baada  ya uchaguzi mkuu.

Wamesema baada ya uchaguzi kufanyika kwani  wanachodai kuwa mgodi  huo umefunguliwa kisiasa  ili viongozi  husika wapate kura kupitia wachimbaji  hao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti  baadhi  ya wachimbaji walisema wamekuwa wakipata taarifa  baada  ya kumalizika kwa shuguli ya kupiga kura mwezi Octoba 25, mwaka huu  kwa kuwapata Diwani,Mbunge na Rais mgodi  huo utafungwa .

Juma Ramadhani  mchimbaji  alisema kuna kila sababu  ya wachimbaji hao kuwaeleza ukweli ili wajue jinsi  ya uwekezaji  wao  kutokana na kutimuliwa mara mbili mgodini hapo hali iliyopelekea  kupata hasara kubwa ya  mali zao.

Alisema taarifa wanazoendelea  kuzipata nikuwa pindi uchagugi utakapo malizika jeshi la polisi litapewa jukumu la kuwafukuza wachimbaji  hao na kuongeza serikali  inapaswa kuwaangalia watu hao kwa jicho  la kuwasaidia  ili waweze kupata ridhiki.

Joseph  Ngullumwa ni mtaalam  wa miamba  akizungumza na wachimbaji hao walipowatembelea  alisema mgodi  huo unatambulika kupitia Ressein ya Tumain  Group  na kuwatoa hofu wachimbaji  hao uhai wa Ressein hiyo  ni miaka saba.

Alisema kuwa mgodi  huo haupo kisiasa  bali unatambulika kisheria na serikali  na kuwataka kufanya  kazi  kwa kujituma ili kujikwamua na umasikini  na kuongeza kuwa serikali  imewekeza kwa wachimbaji wadogo.

Ngassa  Kagune mtaalam  wa miamba aliwataka wachimbaji  hao kuzingatia utunzaji wa mazingira katika mgodi  huo kulipa kodi kama ilivyo ada ilikuweza kukidhi vigezo vya ressein  hiyo ambayo itadumu kwa muda wa miaka saba.

Katibu wa Mgodi  huo Samweli  Nhindilo aliwatoa  hofu wachimbaji hao kuwa Ressein  hiyo ina uhai wa miaka saba na kuongeza kuwa miaka saba ikiisha kuna uwezekano mkubwa wakuihuisha ili kazi ziendelee  kama kawaida.

Aliwataka wachimbaji  hao kufanya kazi kwa bidii  kwa kujituma na kujiamini  kutokana na uwekezaji  huo kuwa ni mkubwa na unatambulika na serikali.

No comments:

Post a Comment